Wakati mmoja Nilianza shughuli kubwa miongoni mwa wanadamu, lakini hawakutambua, kwa hivyo ilinibidi Nitumie neno Langu ili kuwafichulia. Na hata hivyo, mwanadamu bado hangeweza kuyaelewa maneno Yangu, na akasalia kutojua malengo ya mpango Wangu. Na hivyo kwa sababu ya kasoro na dosari za mwanadamu, alifanya mambo ili kukatiza mpango Wangu wa usimamizi, na pepo wachafu wakachukua nafasi ya kujidhihirisha, wakawafanya wanadamu kafara wao, mpaka wakateswa na pepo hao wachafu na wakachafuliwa kila mahali. Ulikuwa wakati huu ambapo Niliona nia ya mwanadamu na kusudi lake. Nilishusha pumzi kutokana na kushindwa kuelewa: Ni kwa nini sikuzote lazima mwanadamuatende kwa ajili ya maslahi yake? Je, kuadibu Kwangu hakukusudii kumkamilisha? Je, Najaribu kumvunja moyo? Lugha ya mwanadamu ni nzuri sana, na nyororo, lakini mat ... Read more »

Views: 117 | Added by: flickrpinquorettfb | Date: 06.23.2019 | Comments (0)