Watu hukodolea macho kila mwendo Wangu, kana kwamba Nakaribia kuleta mbingu chini, na wao kila mara hukanganyikiwa na shughuli Zangu, kana kwamba matendo Yangu ni yasiyoeleweka kabisa kwao. Hivyo, wao hufuata nyayo Zangu kwa yote watendayo, wakiogopa sana kwamba watakosea Mbinguni na kutupwa katika "ulimwengu wa wenye kufa." Sijaribu kuwashikilia watu, bali Huufanya upungufu wao lengo la kazi Yangu. Wakati huu, wanafurahia sana, na kuja kunitegemea Mimi. Ninapotoa kwa mwanadamu, watu hunipenda Mimi jinsi wayapendavyo maisha yao wenyewe, lakini Niulizapo vitu kutoka kwao, wao hujitenga na Mimi. Ni kwa nini? Hawawezi hata kutia katika matendo "haki na akili” ya ulimwengu wa mwanadamu? Kwa nini Natoa matakwa kama hayo kwa watu tena na tena? Je, ni kweli kwamba Sina chochote? Watu hunichukulia Mimi kama mwomba ... Read more »

Views: 133 | Added by: flickrpinquorettfb | Date: 06.22.2019 | Comments (0)