5:36 PM
Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

70. Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

Tong Xin Mkoa wa Fujian

Nilizaliwa vijijini. Nilitoka kwa nasaba ya wakulima wanyenyekevu na zaidi ya hayo familia yetu ilikuwa na watu wachache, kwa hiyo mara nyingi tulikuwa tunadhulumiwa. Nilipokuwa na umri wa miaka 13, kulikuwa na mtoto aliyepigwa na mtu fulani kutoka nje ya kijiji chetu. Wanakijiji walimlaumu kwa uongo baba yangu kwa kuchochea hilo na wakasema walitaka kupekua nyumba yetu na kuchukua ngawira mali yetu, kuchukua nguruwe wetu na hata kumpiga baba yangu. Kulikuwa na wakati pia ambapo mwanakijiji mwingine alichukua wavu wetu wa uvuvi na kuuweka kama wake mwenyewe. Wakati baba yangu alipokwenda kuurudisha, mwanakijiji huyo kwa kweli alimgonga baba yangu, akitegemea nguvu na ushawishi wake mwenyewe. Baba yangu alilazimika kujidhalilisha tu kwa kuwa alijua kwamba hakuwa na fedha wala nguvu. Mama yangu akawaambia ndugu zangu wa kiume nami kwamba ni lazima tujipiganie wenyewe katika siku zijazo, na kamwe tusiishi maisha ya ukandamizwaji kama huu. Nikiwa mchanga na mwenye kuchukia udhalimu katika jamii, nilidhamiria kuwa siku zijazo ningejitokeza na kuwa bora kuliko wengine na kupata heshima yao, na kamwe nisikandamizwe. Kwa hiyo nilisoma kwa bidii sana, lakini sikuwa mwerevu kutosha na sikuweza kuingia katika vyuo vikuu vyovyote, kwa hiyo nilichagua kufuatilia maendeleo katika jeshi na kujiunga kwa urahisi kwa njia ya ahali.

Wakati kwanza nilijiunga, nilisombera kuchukua kazi zote ngumu na chafu na kuonyesha uamilifu wangu kuwavutia viongozi wangu na kupandishwa cheo katika siku zijazo. Hata hivyo, bila kujali nilijaribu kwa bidii kiasi gani, sikuweza hata kupata nafasi ya kiongozi wa kikosi. Pia nilitaniwa na kudhulumiwa daima na wanajeshi wenza kwa sababu ya nguo zangu chakavu na iktisadi, jambo ambalo lilizidisha tu hamu yangu ya kujitokeza. Baadaye, kwa kuegemea ushauri kutoka kwa mwanakijiji mwenzangu, nilijifunza kwamba tathmini na kupandishwa cheo katika jeshi havitegemei kazi ngumu, lakini badala yake ni utoaji zawadi. Ingawa niliona kitu cha aina hii kikiwa chukizo, ilinibidi nichukue njia ya pekee ya kupandishwa cheo. Kwa hiyo, nilidhamiria kuchukua akiba yangu yote ili kutoa zawadi kwa viongozi wangu na kufanya miunganisho; baada ya hapo niliweza kujiandikisha katika chuo cha kijeshi. Lakini baada ya kuhitimu, nilipewa kazi kupika katika kantini kwa sababu sikuwa na fedha za kutosha za kutoa zawadi, na baadaye nikawa Afisa wa ugavi, lakini kwa jina tu. Baada ya miaka kadhaa ya maisha ya kijeshi, nilielewa kuwa warasimu hawakuwaadhibu watoa zawadi na huwezi kufanikisha chochote bila ya kujipendekeza sana kwao. Ukitaka kuendelea, unapaswa kujaribu kila njia za kutengeneza pesa na kutoa zawadi, vinginevyo huwezi kufanikisha chochote bila kujali uwezo wako ni mkubwa kiasi gani. Ili kufanikisha hamu yangu ya kupata, nilianza kutengeneza pesa na kuchangisha fedha kila mahali: Nilitaja bei ya juu na kutia chumvi kiasi kwa makusudi wakati wa kununua chakula, nikipata pesa kidogo ya ziada ya haramu; kuona Afisa wa ugavi wengine wakiuza mchele, niliuza kwa siri lori moja ya mchele kutoka kwa jeshi na kutengeneza yuan elfu kadhaa, na kadhalika. Ingawa nilikuwa nimemwamini Yesu tangu utotoni na nilifahamu wazi kwamba vitu hivi nilivyokuwa nikivifanya vilikuwa ni uhalifu, nilikuwa pia na wasiwasi daima kuhusu kupatikana na kuhukumiwa siku moja, nia ya kupandishwa cheo ilinielekeza kufanya mambo hayo kinyume cha dhamiri yangu. Mara nilipokuwa nimekwisha kuweka akiba pesa kiasi, nilianza kuwapendeza viongozi wangu na kuwapa zawadi zilizowaauni kwa upendeleo wao. Kila wakati kiongozi fulani alipokuja kuniona ningejishughulisha nikienda kunywa pombe naye, kuimba, kuwasiliana na makahaba …. Nilifanya kila kitu kilichowezekana ili kujipendekeza kwake. Nilijaribu kumpendeza kwa njia yoyote iliyowezekana. Wakati wowote viongozi walipohitaji msaada fulani, nilifurahi kuwapa huduma zangu. Yeyote aliyekuwa na uhusiano mzuri na viongozi hao, ningejaribu kuwa karibu naye ili kupata pendekezo zuri. Katika miaka hiyo, nilipanda haraka hadi kwa cheo cha kamanda wa batalioni kwa kukimbilia aina hii ya falsafa ya kidunia. Hatimaye nilijitokeza na niliweza kurudi nyumbani kwa utukufu! Baada ya hapo, kila wakati niliporudi nyumbani, wanakijiji wangenizunguka, wakinipendeza na kunisifu, jambo ambalo liliridhisha majisifu yangu sana. Malengo yangu na tamaa zangu zilikua wakati huo. Kama vile watu wangesema, “Maafisa wengine wana yatetea masilahi yao wenyewe tu, sio umma,” “Tumia mamlaka ukiwa nayo, kwa sababu yakishaondoka, huwezi kuyatumia,” na “Hakuna kitu kama afisa ambaye hahongeki.” Kwa hiyo, nilianza kufurahia marupurupu ya kuwa afisa. Ningepata vitu vya bure popote nilipoenda, na kama mtu angetafuta msaada kutoka kwangu, ningewataka wanipe zawadi na singewasaidia kama zawadi zilikuwa duni. Nilianza kufuatilia chakula na mavazi ya kupendeza, na kuanza kujidai. Nikitegemea ukweli kwamba nilikuwa kama “mtoto wa bidii anayependwa na wote” nikijuana na viongozi muhimu kama kamanda na kamissa wa kisiasa, hata nikawa na kiburi sana hivi kwamba ningewadhulumu watu kwa kuringia uhusiano wangu na wenye nguvu, kuomba zawadi kutoka kwa wasaidizi wangu nikitumia majina ya viongozi hawa. Hivi ndivyo jinsi nilivyopotoka kutoka kuwa kijana sahili Mkristo wa mashambani hadi kuwa mtu mwenye tamaa, mwenye udanganyifu na mwenye majivuno.

Nikiwa mpotovu na aliyeanguka, hata nilionyesha asili yangu ya kuogofya kwa wengine. Mara nyingi nilishuku bila sababu nzuri kwamba mke wangu mrembo ambaye alifanya kazi kwa kampuni ya kigeni alikuwa na uhusiano wa kando; hili lilisababisha mgogoro zaidi kati yetu na utengano uliokuwa ukizidi. Mnamo mwaka 2006, mambo yalimzidi sana mke wangu na akaanzisha mchakato wa talaka; hili lilikuwa kama fedheha kubwa kwangu, hivyo singelikubali. Usiku wa manane daima ningekuwa nikifikiri kuhusu maisha yangu. Nilifikiri mwenyewe: Nimekuwa nikidhamiria kujitokeza tangu utotoni na mke wangu na mimi sote tumefanikiwa katika kazi zetu. Hali katika nyumba yetu ni nzuri kwa kila njia na watu wengine wanatuonea wivu, hivyo kwa nini ninaishi katika maumivu kama hayo, na kwa nini imefika kiasi kwamba mke wangu anataka kunitaliki? Hata mwana wetu wa kiume anateseka pamoja nasi. Je, maisha yangu yako jinsi ninavyotaka yawe? Ninaishi hasa kwa sababu ya nini? Nilipokuwa tu nikihisi kupotea na kuchanganyikiwa, mke wangu aliukubali wokovu wa Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Kwa njia ya mikutano ya mara kwa mara na ushirika na ndugu wa kike na wa kiume, akawa mwenye matumaini mema zaidi na zaidi, aliacha kubishana nami, na kamwe hakutaja talaka tena. Badala yake, alijishughulisha na kuihubiri injili na kutimiza wajibu wake. Baadaye, nikielekezwa na mke wangu na mama yangu, pia nilianza kumwamini Mwenyezi Mungu.

Kwa sababu ya maisha katika kanisa, nilielewa kwamba Mungu ni mtakatifu na mwenye haki, na kwamba Yeye huchukia zaidi uchafu na upotovu wa wanadamu. Nilifikiria njia chafu ambazo kwazo nilikuzwa katika jeshi na kwamba labda singeweza kuokolewa na Mungu kama singebadilisha tabia yangu ya zamani, hivyo nikaanza kusoma maneno ya Mungu kwa shauku, nikitumaini kuwa ningeweza kupata suluhisho ndani yayo. Siku moja, nilisoma maneno haya kutoka kwa Mungu: “Kwa sababu ya kuzaliwa katika nchi ya uchafu vile, mwanadamu ameangamizwa kabisa na jamii, amekuwa akishawishiwa na maadili ya kikabaila, na amefundisha katika ‘taasisi za elimu ya juu.’ Fikra zilizo nyuma kimaendeleo, maadili potovu, mtazamo mbaya juu ya maisha, falsafa za kudharauliwa, uwepo usio na thamani, na hali ya maisha potovu za maisha na desturi—mambo yote haya yameuingilia moyo wa mwanadamu, na kudhoofisha na kushambuliwa dhamiri yake pakubwa. Matokeo yake, mwanadamu kamwe yuko mbali kutoka kwa Mungu, na kila mara anampinga” (“Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalifichua siri katika asili ya moyo wangu; nilitetemeshwa vibaya. Miaka yote ya kuhudumu kati jeshi, nilikuwa nimefuata “sheria zisizosemwa” za ulimwengu kwa ajili ya kujitokeza. Nilikuwa nimefanya mambo mengi ambayo yaliisumbua dhamiri yangu. Nilikuwa nimekuwa tajiri kutokana na mapato yasiyo halali na kuishi maisha ya giza na mapotovu—siku zote nilijiingiza katika dhambi lakini sikuona haya. Halafu, maneno ya Mungu hayakuniruhusu tu kutofautisha mema na mabaya, bali pia yalinifanya nione kwa dhahiri asili ya kuanguka kwangu na upotovu wangu. Ilielekea kuwa mabaa haya yalitoka kwa Shetani. Ilikuwa ni Shetani aliyegeuza nchi hii kuwa kinamasi cha uovu na ukatili ambapo watu wasiokuwa na nguvu na waliokuwa waaminifu walikandamizwa na walijitahidi kuishi huku walio na nguvu, ushawishi na wenye udhalimu walisitawi. Katika jamii hii kulijaa uasi na uongo kama “Kila mtu ajitetee mwenyewe bila kujali jaala ya wengine,” “Maafisa huwa hawafanyi mambo kuwa magumu kwa wale ambao hubeba zawadi,” “Huwezi kufanikisha chochote bila kujipendekeza sana kwao,” “Baadhi ya maafisa wanazingatia tu masilahi yao, sio umma,” “Tumia mamlaka ukiwa nayo, kwa sababu yakishaondoka, huwezi kuyatumia,” na kadhalika. Nilidanganywa na misemo hii ya kuogofya, na kwa sababu ya ukandamizaji karibu nami nilipoteza njia yangu, nikaziacha kanuni za kibinadamu, kutafuta vyeo vya juu kwa njia isiyo na maadili, na nikafanywa madhubuti katika kinamasi cha dhambi. Hatimaye nikawa mtu mwovu ambaye hakutafuta chochote ila utajiri, nikatumia mamlaka vibaya kwa faida ya kibinafsi, na kufuja fedha za umma. Kutoka kwa hukumu katika maneno ya Mungu, niliona ghadhabu kali na utakatifu wa Mungu, na kuelewa kuwa kukosea tabia Yake ya haki haikuruhusiwa. Nilijutia vitendo vyangu viovu na moyo wangu ulijazwa hofu. Nilihisi kwamba kama haingekuwa kwa ajili ya Mungu kuniokoa wakati ufaao na kunivuta kutoka kwa kinamasi cha uovu, ningelaaniwa na kuadhibiwa na Mungu kwa sababu ya yale niliyoyatenda. Asante Mungu kwa kuniruhusu nione mwanga tena, na kuelewa kanuni za binadamu. Kuanzia wakati huo na kwendelea, sikuwahi tena kamwe kufanya mambo hayo yaliyoleta aibu kwa jina la Mungu.

Nilipoelewa ukweli zaidi na zaidi, nilipitia wokovu zaidi na wa kina kutoka kwa Mungu. Katika mwaka wa 2009, nilikuwa nimehudumu katika jeshi kwa miaka 20. Kwa mujibu wa kanuni za kitaifa, niliruhusiwa kwenda nje na kutafuta kazi mimi mwenyewe. Nilidhamiria kuepukana na uovu na kufanya mema, kwa hiyo nikaacha jeshi na kuchagua kuhamishwa hadi kwa kazi ya raia, na kuweka moyo wangu na nafsi yangu katika kufanya kazi kwa ajili ya Mungu. Hata hivyo, kiongozi wangu alijaribu kunishawishi kukaa na kuniuliza kulifikiria kabisa, na kiongozi mwingine mzee wa cheo cha juu alinipa ahadi ya kuwa ningepandishwa cheo kuwa kamanda wa rejimenti kama ningeendelea kufanya kazi kwa bidii. Nilisita kidogo—hii ilikuwa ndiyo fursa ambayo niliitamani usiku na mchana! Sikuweza kuachilia wazo la cheo hicho, hivyo nilitafuta msaada kutoka kwa Mungu na kuomba, “Ee, Mungu, kuwa katika cheo cha juu kumekuwa ndoto yangu daima. Sasa nina fursa hiyo na sijui jinsi ya kuchagua. Tafadhali nipe nuru na kuniongoza!” Maneno yafuatayo ya Mungu yaniletea nuru, “Kama wewe ni wa daraja la juu, wa sifa ya heshima, aliyemiliki maarifa mengi, mmiliki wa mali nyingi, na kuungwa mkono na watu wengi, lakini mambo haya hayakuzuii kuja mbele za Mungu kuukubali wito Wake na agizo Lake, kufanya kile Mungu anachokuambia ufanye, basi yote unayoyafanya yatakuwa yenye umuhimu zaidi duniani na yenye haki zaidi ya binadamu. Ukiukataa wito wa Mungu kwa sababu ya hadhi yako na malengo yako mwenyewe, yote utakayoyafanya yatalaaniwa na hata kudharauliwa na Mungu” (“Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Watu huja duniani na ni nadra kupatana na Mimi, na pia ni nadra kuwa na fursa ya kutafuta na kupata ukweli. Kwa nini msithamini wakati huu mzuri kama njia sahihi ya kutafuta katika maisha haya?” (“Maneno kwa Vijana na Wazee” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kila neno la Mungu lilipiga dhamiri yangu, na nilizinduliwa kutoka kwa kusita kwangu. Nilikuwa na faida kubwa ya kukutana na kazi iliyo duniani ya Mungu mwenye mwili na fursa ya thamani ya kutafuta ukweli na kufanya kazi kwa Mungu. Ni kuinuliwa kweli na neema kutoka kwa Mungu! Ni kazi gani ulimwenguni inaweza kuwa na maana zaidi kuliko kufanya kazi kwa Muumba? Hata kama ungekuwa na madaraka ya juu na ungekuwa afisa wa kiwango cha juu zaidi, ikiwa hukumjua Mungu na hukuwa umefanya mabadiliko yoyote katika tabia yako, hatimaye ungeadhibiwa na Mungu. Watu wengi katika vyeo vya kifahari walikuwa wameanguka katika maafa na kufa kifo cha mapema, na viongozi wengi wa vyeo vya juu walikuwa wamepata maanguko ya aibu na hatima ya kuogofya. Kwa upande wangu, nilikuwa nimepambana na kujaribu bila tumaini kujitokeza kama afisa, hayo yakinisababishia kujiharibu kwa kiwango kwamba nilikuwa na waa na uchafu, na kuishi maisha ya mtu ambaye hakuwa binadamu kamili. Mungu kisha akaniongoza nyuma kutoka kwa njia mbaya na kwa dhahiri alinionyesha njia ya maisha ya kibinadamu. Ningewezaje bado kuchagua kuchukua mambo hayo ya hatari na kurudi kwa njia zangu za zamani? Nusu ya kwanza ya maisha yangu ilikuwa yenye uelekeo wa mateso ya Shetani na udanganyifu na iliniletea maumivu makubwa. Sikuweza kufanywa mtumwa, kutumiwa, na kupotoshwa na Shetani kwa nusu ya mwisho. Ilinibidi kubadilisha njia yangu ya kuishi, kumfuata Mungu kwa udhabiti, kuitembea njia ya kutafutilia ukweli, na kuishi maisha yenye maana. Kwa hivyo kwa ushupavu nilidhamiria kutafuta kazi mimi mwenyewe na kuondoka jeshini kabisa. Hata hivyo, kwa sababu upotovu wangu kutoka kwa Shetani ulikuwa mkubwa sana, wazo lake la sumu la kujitokeza na kuwa mtu muhimu lilikuwa limekita mizizi moyoni mwangu na mara nyingi lilinizuia kuchukua njia iliyo sahihi. Mungu alikuwa amefanya kazi hata zaidi ya hukumu na kutakasa ndani yangu ili kuniongoza kwa njia ya kweli katika maisha, na nilipokea hata wokovu zaidi kutoka kwa Mungu.

Baada ya kutimiza wajibu wangu kanisani kwa muda fulani, niliona kuwa baadhi ya viongozi wa kanisa walikuwa wachanga sana na mmoja wao alikuwa rafiki yangu, jambo lililonifanya kuhisi kuwa na wasiwasi sana. Nilifikiri: Hakuna vyeo vyovyote vyenu katika ulimwengu wa kidunia vilikuwa vya juu kama vyangu, lakini vyeo vyenu vya sasa katika kanisa ni vya juu kuliko vyangu. Kama mna uwezo wa kuwa viongozi, basi mimi ninao hata zaidi! Kwa hiyo nilifanya bidii katika ukimbizaji huu; niliamka saa kumi na moja kila asubuhi kusoma maneno ya Mungu, na kujiwekea malengo—kusikiliza mahubiri na ushirika juu ya kuingia katika maisha angalau saa mbili kila siku, kujifunza nyimbo tatu kila wiki, na kupanga kujifunza nyimbo zote za neno la Mungu. Nilifanya bidii hata zaidi katika kutekeleza wajibu wangu kanisani. Mradi kilikuwa ni kitu ambacho nilikuwa na uwezo wa kukishughulikia kanisani, ningepuruka kukifanya bila kujali jinsi kilivyokuwa kigumu au cha kuchosha. Wakati ule ule, nilijigambia uzoefu wangu na ujuzi katika jeshi mbele ya ndugu zangu wa kike na wa kiume, nikaonyesha dharau kwa mawasiliano ya viongozi wa kanisa au kwa werevu nikadunisha jinsi walivyoyachukulia maswala au kuyashughulikia matatizo. Kwa hiyo, nilisonga kabisa mbele kwa haraka, nikijitahidi kujitafutia umaarufu, nikitumainia kupata cheo rasmi katika kanisa haraka iwezekanavyo. Katika mwaka wa 2011, hatimaye nilichaguliwa kuwa kiongozi katika kanisa kama nilivyotarajia. Nilifurahi sana na nilitayarisha kujibainisha na kufanikisha mambo mengi makubwa ili kuwavutia wengine. Hata hivyo, mke wangu alinikumbusha mara nyingi kwamba sikufaa kuwaongoza wengine na akanishauri kuwa nijiuzulu. Sikuwa na chaguo ila kujiuzulu na nikampendekeza dada fulani kama kiongozi. Hata hivyo, sikuwa nimekubali kuvumilia hili ndani ya moyo wangu. Baada ya muda fulani, niliona kwamba huyo kiongozi alikuwa na dosari fulani katika jinsi alivyoshughulikia matatizo, na tamaa yangu tena iliibuka. Nilimpendekezea kwa njia isiyo dhahiri kwamba awajibike na kujiuzulu, jambo ambalo lingenipa fursa ya kuchaguliwa katika uchaguzi uliofuata. Hata hivyo, ndugu wa kike na wa kiume waliopata habari hii walinichunguza, wakisema kuwa nilikuwa mjanja na mwenye tamaa sana, na kwamba daima nilitaka kuchukua udhibiti wa kanisa, kwa hiyo walinifukuza kutoka kwa cheo changu cha kiongozi wa kikundi. Sikuweza kabisa kulikubali. Nilikuwa mtu mwenye uwezo mno; ingewezekanaje kuwa sikuwa hata wa kufaa kuwa kiongozi wa kikundi! Kwa miezi kadhaa, nilikuwa wa kutoridhika sana katika moyo wangu na sikuwa na furaha na ndugu zangu wa kike na wa kiume, kwa hiyo sikuzungumza sana katika mikutano. Roho yangu ilijaa giza na sikuweza kumtafuta Mungu. Katikati ya maumivu haya, nilimwomba Mungu anitoe kwa giza hilo. Na siku moja, nilisoma maneno ya Mungu, “Leo, katika uzoefu wa mwanadamu, kila hatua ya kazi ya Mungu inayagonga mawazo ya mwanadamu, na kila hatua haiwezi kuwazwa na akili ya mwanadamu, na kuzidi matarajio ya mwanadamu. Mungu Anakimu mahitaji yote ya mwanadamu, na kwa kila njia yote huwa yanakinzana na mawazo ya mwanadamu…. Kwa kuzigonga fikira zako, unakuja kukubali kazi ya Mungu, na kwa njia hii pekee ndio unaweza kuondoa upotovu wako” (“Wale Wanaomjua Mungu Pekee Ndio Wanaoweza Kuwa na Ushuhuda Kwa Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Usipotii sasa, hatimaye utalaaniwa—utafurahi wakati huo? Huzingatii njia ya maisha lakini unalenga tu hadhi na jina lako; je, maisha yako yakoje? … Hulengi kufuatilia mabadiliko ya kibinafsi na kuingia ndani; daima wewe hulenga tamaa zile badhirifu na vitu vinavyozuia upendo wako kwa Mungu na kukuzuia kufika karibu na Yeye. Je, vitu hivyo vinaweza kukubadili? Je, vinaweza kukuleta katika ufalme?” (“Mbona Huko Tayari Kuwa Foili[a]?” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno makali ya Mungu ya hukumu yaliudunga moyo wangu, ukinifanya mwasi mimi kuona aibu na tahayari. Ni wakati huo nilipotambua kwamba vitu vyote vilivyonipata karibuni, huku vikiwa sivyo nilivyotaka, havikuwa na maana kwamba watu walikuwa wanafanya mambo kuwa magumu kwangu tu. Badala yake, vilikuwa tu hukumu ya haki yangu kutoka kwa Mungu, na wokovu Wake kwangu wa wakati ufaao. Kazi ya Mungu wakati huo ilikuwa na maana ya kubadilisha mawazo na mitazamo ya kale ya watu, ili kuwaokoa kutoka kwa ushawishi wa Shetani, na wao kupata ukweli na uzima kutoka kwa Mungu na kuishi maisha ya furaha. Sikuchukua njia sahihi na kutafuta kupata ukweli kama maisha yangu, lakini nilifuatilia hadhi na umaarufu, na hata nilifanya hila na kula njama, sio tofauti na ukimbizaji wa kuwa afisa na mtu wa umuhimu. Si hiki kilikuwa kinyume na kazi ya Mungu na mapenzi Yake ya kuwaokoa wanadamu? Ningewezaje kupata ukweli na kuishi maisha yenye maana ikiwa ningeendelea kufuata haya? Kama singekuwa nimerudi nyuma, si lingekuwa limenidhuru na kunifanya shabaha ya adhabu na Mungu Amalizapo kazi Yake? Kupitia kwa wale waliokuwa karibu nami, Mungu alivipogoa vipengele vyangu na kunishughulikia “kwa ukatili,” akaondoa hadhi yangu, na kuangamiza matamanio yangu na tamaa ili kunizuia kuchukua njia mbaya, kurekebisha mawazo yangu ya ukimbizaji yaliyokuwa na dosari, na kunifanya nirudi nyuma. Kisha nikaelewa tabia ya haki na takatifu ya Mungu, na kwamba nia zangu, motisha, na hata kila wazo na kitendo vyote vilikuwa chini ya uchunguzi Wake. Mungu alifanya wokovu wa kweli zaidi kwangu wakati ule ule ambapo alionyesha uadhama Wake. Baada ya kutambua neema ya wokovu wa Mungu, sikujiruhusu tena kutegwa katika upotezaji wa hadhi, na nilikuwa na hiari ya kufuatilia ukweli. Mungu alinipenda sana kiasi kwamba Alijaribu kuniokoa, kwa hiyo sikuweza kumsikitisha. Nililazimika kuitii mipango ya Mungu, na bila kujali kama nilikuwa kiongozi au mlei, nilipaswa kufuatilia ukweli na kufanya wajibu wangu vizuri iwezekanavyo.

Nusu mwaka baadaye, kiongozi katika kanisa alinipangia kuendelea na maisha yangu ya kanisa kwa kanisa jingine. Viongozi wa kanisa walikuwa wakichaguliwa wakati huo. Nilipogundua kuwa nilikuwa nimemwamini Mungu kwa muda mrefu kuliko ndugu wote wa kike na wa kiume, nilifurahi sana na nikafikiri: Sasa fursa yangu imewadia. Hatimaye naweza kuonyesha uwezo wangu kama kiongozi. Zaidi ya yote, nina uzoefu zaidi wa maisha na nilimwamini Mungu kabla yao. Mimi ndiye mtu bora zaidi kwa cheo hicho. Nilipokuwa nikijiandaa kujitambulisha kwao vizuri, mmoja wa dada kutoka kanisa la awali alihamishwa kujiunga na uchaguzi. Niliogopa kwamba angefichua kashfa yangu ya awali ya kushindania madaraka, ambayo ingekuwa tahayari kwangu, hivyo ilinipasa kusalimisha mpango wangu wa awali. Niliamua kujaribu kuchaguliwa kama kiongozi wa kikundi, kisha nijitahidi kupanda ngazi hatua kwa hatua baada ya hapo. Sikuwa nimedhani kuwa singechaguliwa kama kiongozi wa kikundi, lakini badala yake ningepangiwa kufanya kazi fulani ndogo ambayo ilihitaji kupeleka vitabu vya maneno ya Mungu kwa ndugu wa kike na wa kiume. Mimi, kamanda mheshimiwa wa batalioni, nilikuwa nikikurupua huku na kule nikifanya kazi ndogo za kutumwa. Niliona hili likiwa gumu kukubali. Hata hivyo, baada ya kupitia hukumu na adabu ya Mungu, nilielewa kuwa hili lilikuwa kutoka kwa utawala wa Mungu na mipango Yake. Mungu alikuwa akiishughulikia tamaa yangu ya kufuata hadhi, hivyo nikajinyima na kutii. Hata hivyo, baada ya muda mfupi mahali nilipohudhuria mikutano paligunduliwa na polisi, hivyo kanisa liliniandalia kukutana na dada wengine wawili wazee mahali pengine. Kwa mintarafu ya kiongozi wa kanisa, hakuweza kuja mara nyingi sana kutekeleza wajibu wake wa kunyunyizia kwetu kwa kuwa alikuwa akiteswa na Chama cha Kikomunisti cha China. Wakati huo, sikuweza kulivumilia tena: Mbali na kunitaka nifanye kazi ndogo ndogo, nilipaswa kukutana na wazee wenye ubora duni wa tabia. Nilipataje kuwa mahali hapa? Nilivyozidi kulifikiria, ndivyo nilivyozidi kujihisi vibaya zaidi. Hata nilihisi kwamba maisha hayakuwa na thamani kuyaishi. Katika maumivu, nilisali kwa Mungu kwa bidii na kumwomba anipe nuru Yake. Siku moja, nilisoma maneno ya Mungu, yakisema, “Ni mbinu gani iliyo ya kufaa zaidi ya ufukuziaji katika njia ya leo? Ni umbo la aina gani unalopaswa kujiona mwenyewe kama katika ufukuziaji wako? Unapaswa kujua namna ya kushughulikia kila kitu kinachokufika wewe sasa, yawe ni majaribio au mateso, kuadibu bila huruma au laana—unapaswa kufikiria kwa makini haya yote” (“Je, Wale Wasiojifunza na Wasiojua Chochote si Wanyama tu?” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kutoka kwa maneno ya Mungu, nilielewa kuwa niliongozwa na asili yangu ya kiburi ya kishetani, nikachepuka kutoka kwa mapenzi ya Mungu, na nikatembea kwa njia mbaya ya kutafutilia umaarufu na vyeo. Kwa sababu hiyo, niliyaona tu majukumu yale yaliyo na “majina rasmi” kuwa muhimu na kuyadharau majukumu mengine, na hata nikawachukia wale ndugu wa kike na wa kiume wa ubora duni wa tabia kwa maana ya kwamba nilihisi hadhi yangu ilikuwa ikidunishwa kwa kuwa nao. Hadhi, umaarufu na utajiri vilikuwa vimeingia kichwani mwangu. Hata hivyo, sikujua kwamba katika nyumba ya Mungu, majukumu yote yalikuwa sawa, na ndugu zangu wa kike na wa kiume na vilevile mimi sote tulikuwa viumbe waliokuwa na hali sawa. Hadhi yangu ya juu katika ulimwengu wa kidunia haikuweza kubadilisha kamwe ukweli huo. Kufikiria hili, nilihisi nimefarijika sana. Hata hivyo, nilijua kuwa umaarufu na hadhi vilikuwa ni udhaifu wangu, hivyo nilimwomba Mungu kutafuta ukweli zaidi ili kutatua suala hili. Baadaye, nikasikia baadhi ya mahubiri yakitoa ushirika juu ya kuingia katika maisha, yakisema: “Kwa maoni yako, ina maana kwa watu kuwa na vyeo na kuvitunza? Unapaswa kuona vizuri sana hadhi na umaarufu na kutovijali. Ni vitupu na havina maana. Cheo cha juu hakihakikishi baraka. Kama huna tabia nzuri, cheo cha juu kinaweza kukuletea balaa. Usipofuatilia ukweli, hicho cheo kitakuwa chanzo cha uovu mkubwa kwako. Bila ukweli, huwezi kuona vitu vizuri sana, na huenda ukaangamizwa kwa urahisi na vyeo. ... Huwezi kuwa kiongozi bila kufuatilia ukweli; inaweza tu kukuangamiza. Ukifuatilia ukweli, uongozi unaweza kukufanya mkamilifu” (“Utofautishaji wa na Ufumbuzi kwa Viongozi wa Uongo, Wapinga Kristo na Waovu” katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha VII). “Watu huonekana kuwa wema wakati hawana mamlaka lakini mara tu wanapoyapata, wataonyesha silika zao za kweli. Mamlaka yanawezaje kuwafichua watu? Wakati mtu ni wa kawaida, yeye huonekana kuwa mwenye heshima na huonekana kuwa mwadhamu na mwadilifu. Mara anaposhikilia mamlaka kiasi, anakuwa kaidi” (“Jinsi Watu Wanavyopaswa Kushirikiana na Kazi ya Mungu ya Kumkamilisha Mwanadamu” katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha III). Maneno haya ghafla yalifungua macho yangu na nikaona utupu na hali ya kutokuwa na maana ya kufuatilia hadhi. Kuthamini hadhi na kushindwa kufuatilia ukweli kunaweza tu kuwaelekeza watu kwa maangamizi. Chukua uzoefu wangu katika jeshi kama mfano—niliwachukia hao maofisa wapotovu wakati nilipokuwa askari. Hata hivyo, hadhi yangu ilipoendelea kukua, niligeuka kuwa afisa mpotovu kweli. Wale ambao walikuwa katika vyeo vya juu walionekana kuwa wema na waaminifu wakati hawakuwa na hadhi ya juu. Hata hivyo, mara tu walipopata mamlaka, walianza kutenda kwa udhalimu na kufanya makosa yasio na idadi. Ukweli huu ulikuwa wa kutosha kuonyesha kwamba baada ya watu kupotoshwa na Shetani, bila ya ubaguzi wangepatwa na mateso na udanganyifu wake; kama hawakufuatilia ukweli na kuwa na mabadiliko katika tabia, wangeweza tu kuwa wapotovu na kufanya uovu mara tu walipokuwa na mamlaka na hadhi, iwe ni katika ulimwengu wa duniani au katika nyumba ya Mungu, matokeo ya mwisho yakiwa ni kuadhibiwa kwa haki na Mungu. Nikifikiri juu ya hili, nilihisi hofu na shukrani. Ilielekea kuwa kuvunjika moyo kwangu kwa mara kwa mara kulikuwa ndio wokovu wangu, uliofanywa kwa sababu ya upendo kwangu! Kwa sababu nilijitahidi kupanda katika ulimwengu wa urasimu kwa miaka mingi, nilikuwa nimechafuliwa na sumu ya Shetani. Inaweza kusemwa kuwa nilikuwa mchanganyiko wa kiburi, hila, ubinafsi na tamaa. Baada ya kumwamini Mungu, niliithamini hadhi mno na kwa kweli sikufuatilia ukweli. Matokeo yake yalikuwa, hata kwa wakati huo nilikuwa nimepata ukweli kidogo, na nilikuwa na hofu kidogo ya Mungu. Kama kwa kweli ningekuwa katika cheo kikubwa, ningekuwa tu na tamaa na kutenda kwa udhalimu kama nilivyofanya katika jeshi, na ningeishia kuadhibiwa kwa kuikosea tabia ya Mungu. Kwa sababu ya kupata nuru ya Mungu, niliweza kuona kwa dhahiri asili na matokeo ya kufuatilia umaarufu na hadhi, na zaidi ya hayo, niliweza kuona umuhimu wa kufuatilia ukweli.

Baada ya hapo nilianza kuweka jitihada zangu kwa maneno ya Mungu. Nilitamani sana maneno ya Mungu kuwa maisha yangu na sikuzingatia wajibu uliokuwa na “majina rasmi,” na kamwe sikudunisha kazi zingine. Nilihisi kwamba kila wajibu ulikuwa na maana yake, kwamba wote ulitawaliwa na kuamuliwa kabla na Mungu, na kwamba wajibu wangu ulikuwa jukumu ambalo napaswa kubeba. Nilipoyatamani maneno ya Mungu kwa moyo wangu wote na kujaribu kukamilisha wajibu wangu, sikuelewa tu ukweli mwingi ambao sikuuelewa kabla, lakini pia niliufurahia uwepo wa Mungu mara nyingi kabisa. Nilipokea nuru na uongozi wa Roho Mtakatifu, ambao ulinifanya kujihisi kupata kuadhibiwa kwa kuzuiliwa na mwenye furaha isiyosemeka. Baada ya kipindi cha muda, nilijikuta nikiwa katika hali ya kuepuka kujulikana wakati nikiingiliana na wengine, na sikujisifu tena juu ya vyeo vyangu vya zamani katika jeshi au kuvitumia kujitangaza. Bila kujali ni nani aliyeonyesha makosa yangu, ningetii kwanza na kujitafakaria baadaye. Niliweza kuwatendea ndugu zangu wa kike na wa kiume katika kanisa waliokuwa na elimu ya chini na ubora wa chini kwa usawa, na mimi sikujiona tena kuwa ni bora kuwaliko. Kabla ya mimi kulijua maoni yangu juu ya ukimbizaji yalibadilika sana, na nikakosa kujali hadhi na umaarufu na sikuzuiwa sana na kudhibitiwa na haya. Nilipoona ndugu wa kike na wa kiume waliomwamini Mungu kwa muda mfupi kuniliko wakichaguliwa kuwa viongozi wa kanisa, nilihisi wivu kidogo. Hata hivyo, niliweza kuliachilia hilo kupitia sala. Nilitahayari nikifikiria ukweli kwamba nilikuwa nikipigania sifa na faida; Nilihisi kuwa lilikuwa jambo baya na katili. Sasa, miye na mke wangu hutimiza majukumu yetu nyumbani pamoja. Ingawa sio majukumu muhimu, mimi huhisi kuridhika na kufurahia. Mwanangu wa kiume sasa anamwamini Mwenyezi Mungu pia, jambo linaloifanya familia yetu kuwa familia ya Kikristo ya kweli ambapo maneno ya Mungu hutawala. Bila kujali ni nani husema kulingana na ukweli, tutamsikiliza huyo mtu. Hata kama kuna ufunuo wa tabia, tunaweza kuelewa, tunaweza kuvumiliana na kusameheana, na kujichunguza kulingana na maneno ya Mungu, jambo ambalo limeifanya familia yetu kuwa na furaha zaidi na zaidi. Ninahisi sana kwamba ni Mwenyezi Mungu aliyetubadilisha mimi na mke wangu, ambaye ameziokoa ndoa yangu na familia yangu, na aidha, ameniokoa kutoka kwa upotovu wa kuzidi kiasi na kunibadilisha kutoka kuwa mwenye kiburi, mwovu na mchafu na mtafutaji wa sifa hadi kuwa mtu ambaye hufuatilia mwanga na haki, ambaye ana malengo halisi ya maisha. Ninaposoma maneno haya ya Mungu, hisia za aina zote huchemka ndani yangu: “Tangu uumbaji wa dunia hadi sasa, yote ambayo Mungu amefanya ni upendo, bila chuki yoyote kwa mwanadamu. Hata kuadibu na hukumu uliyoiona ni mapenzi pia, upendo wa kweli na wa dhati zaidi; upendo huu huwaongoza wanadamu kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu. … Kazi yote Aliyoifanya ni kumwongoza mwanadamu kwenye njia sahihi ya maisha ya wanadamu, ili kwamba wawe na maisha ya kawaida ya wanadamu, kwani mwanadamu hajui jinsi ya kuishi. Bila uongozi kama huo, utaishi maisha tupu yasiyo na maana wala thamani, na kamwe hutajua jinsi ya kuwa mwanadamu wa kawaida” (Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Kushinda (4) katika Neno Laonekana katika Mwili). Ndio, bila ya wokovu wa Mungu, singekuwa nimechukua njia sahihi katika maisha; ningekuwa nimepotoka tu zaidi na zaidi, na ningekuwa nimekwishakuwa mtu duni kabisa na mchafu ambaye angelaaniwa na Mungu mwishowe. Ni hukumu ya haki ya Mungu ambayo imeniokoa, na usafishwaji usio na huruma ambao umenibadilisha. Hili huniwezesha kuelewa lililo baya na lililo takatifu na pia ukuu wa Mungu, uzuri na wema, na ukatili wa Shetani na uovu. Sitamfuata Shetani tena kamwe, na nitafuatilia tu ukweli kikamilifu, kujiondolea upotovu wa Shetani, na kuishi maisha halisi ya kibinadamu. Ingawa nimepitia mateso ya kuadibu kwingi na usafishwaji, nimepata njia ya thamani zaidi ya maisha, ikiniruhusu kuzaliwa upya na kuingia njia ya kweli katika maisha.

Mwaka huu, nilirudi kwa kitengo changu cha kazi cha zamani ili kushughulikia kazi zingine za utaratibu. Niliona kwamba wenzangu wa zamani na viongozi wangu wa awali walikuwa wote wamepandishwa vyeo. Wenzangu wa zamani waliponiona, walisema, “Kama hungeacha jeshi, ungekuwa umepandishwa cheo kufikia sasa.” Nilibaki kutoingiwa na hisi, na nikafikiri: Cheo kikubwa ni cha haja gani? Ukiishi bila lengo lolote, mwongozo au maana kama mtu lakini uvurugevuruge tu katika matope hayo ya uovu, si hayo ni maisha ya kushusha hadhi mno? Si nyinyi ni watumwa wa Shetani tu, wanasesere wake? Utapata adhabu ya haki ya Mungu na malipo hatimaye! Ingawa sina cheo kikubwa, sijuti kamwe uchaguzi wangu, kwa sababu kwa hakika nimepitia amani na utulivu moyoni mwangu, ambao ni furaha ya kweli. Ni kwa kuwa tu kiumbe ambaye unapaswa kuwa, ukimtii na ukimwabudu Mungu ni maisha ya kweli ya binadamu, na ni kwa njia hii tu unapoweza kuwa na mustakabali yenye furaha!

Tanbihi:

a. Mtu/kitu kinachodhihirisha uzuri/ubora wa kingine kwa kuvilinganisha.

Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu

Views: 81 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: Maneno ya Mungu, ukweli, Kanisa | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar