7:40 PM
Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza

Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza

Mo Zhijian Mkoa wa Guangdong

Nilizaliwa katika eneo maskini, la mbali lenye milima ambako tumefukiza na kumwabudu Budha kwa vizazi vingi. Kuna hekalu za Budha sehemu hiyo kote ambako familia zote zingekwenda kuchoma uvumba; hakuna mtu yeyote aliyewahi kumwamini Mungu kamwe. Katika mwaka wa 1995, mimi na mke wangu tulikuwa katika sehemu nyingine ya nchi ambapo tulimwamini Bwana Yesu; baada ya sisi kurudi tulianza kushiriki injili na idadi ya watu ambao waliikubali ilikua polepole hadi watu zaidi ya 100. Kwa sababu watu zaidi na zaidi walikuwa wakimwamini Mungu, liliishtua serikali ya mitaa. Siku moja mwaka wa 1997, polisi waliniita kwenda kituo cha polisi cha mahali palepale, ambapo mkuu wa Ofisi ya Usalama wa Umma ya Wilaya, Mkuu wa Ofisi ya Usalama wa Taifa, mkuu wa Ofisi ya Dini na mkuu wa kituo cha polisi na vilevile maafisa wachache wa polisi walikuwa wananisubiri. Mkuu wa Ofisi ya Usalama wa Umma aliniuliza: “Kwa nini unamwamini Mungu? Wewe huwasiliana na nani? Biblia zilitoka wapi? Kwa nini huwa huendi katika Kanisa la Kanuni Tatu za Binafsi kwa ajili ya mikusanyiko?” Nikasema: “Watu waliumbwa na Mungu, mwanga wote wa jua, hewa, na maji viliumbwa na Mungu; ni sheria ya mbingu na dunia kwamba watu wamwamini Mungu na kumwabudu Yeye. Katiba ya kitaifa pia inasema wazi kwamba wananchi wana uhuru wa dini; kwa nini msituruhusu tumwamini Mungu kwa uhuru?” Mkuu wa Ofisi ya Dini alisema: “Kuna mipaka kwa uhuru wa kidini, kama tu ndege mdogo ndani ya tundu; ingawa mabawa na miguu yake havijafungwa, anaweza tu kusogea ndani ya tundu.” Nilipomsikia akisema hoja hizi za uwongo, nikawa na hamaki na kusema kwa hasira: “Basi serikali ya kitaifa inawadanganya watu wake!” Waliposikia nikisema haya, walijua kwamba walikuwa na makosa na hawakuwa na kitu cha kusema, hivyo waniruhusu tu niende nyumbani. Wakati huo, sikuwa na ufahamu wa kiini cha mateso ya serikali ya CCP ya waumini hadi mwaka wa 1999 wakati nilipoikubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Kwa njia ya kusoma maneno ya Mungu na kupata uzoefu hata zaidi wa mateso katili kutoka kwa serikali ya CCP niliweza kuona wazi kwamba CCP kilikuwa mfano halisi wa Shetani aliye pepo mbaya; kilikuwa adui wa Mungu kama ilivyoelezwa katika Biblia: “Nalo joka kubwa likatupwa nje, yule nyoka mzee, anayeitwa Ibilisi, na Shetani, anayeidanganya dunia nzima” (Ufunuo 12:9).

Baada tu ya saa kumi na moja alfajiri kuu ya Juni 28, mwaka wa 2002, nilikuwa nikijiandaa kwa mkusanyiko na ndugu wengine wa kiume na wa kike tuliposikia ghafla kelele ya kuponda kwa mlango. Tulificha vitabu vya neno la Mungu kwa haraka na kisha tukaufungua mlango. Bila kutarajiwa, mlango ulipofunguliwa, takribani dazeni moja ya polisi walikurupua ndani. Walikuwa na virungu vya umeme na bunduki mikononi mwao na kutulazimisha tukusanyike pamoja, wakitufanya tuchuchumae na kuweka mikono yetu juu ya vichwa vyetu. Baada ya polisi hawa waovu kutudhibiti, kama majambazi wakiingia katika kijiji, waliingia kila chumba na kuvuruga kila kitu; walichukua matandiko na nguo zetu na kuzitupa kote sakafuni. Katika siku za nyuma nilikuwa nimeangalia matukio kwa televisheni ya uhalifu uliopangwa na majambazi wakipora na kuiba, lakini sikutazamia kamwe kuwa “polisi wa umma” wangetenda kama vile tu wadhalimu waovu na majambazi kwa TV. Wakati huo nilikuwa na hofu sana na wasiwasi kwamba wangegundua vitabu vya neno la Mungu. Niliendelea kuomba moyoni mwangu na kumuuliza Mungu atuchunge na kutukinga. Baada ya kuomba, niliona matendo ya ajabu ya Mungu. Walipekua nyumba nzima na kutafuta na kutunyang’anya vitu vyetu binafsi, lakini hawakupata vitabu vya neno la Mungu. Nilijua kwamba huu ulikuwa ni uweza wa Mungu na ulinzi na nilijua kwamba Mungu alikuwa pamoja nasi, na imani yangu kwa Mungu iliongezeka. Baadaye, wakatupeleka kwa kituo cha polisi na wakati wa usiku, walituhamishwa hadi kwa kituo cha kizuizi na kutufungia. Siku tatu baadaye, polisi walitoza kila mmoja wetu faini ya yuan 300 ambazo tulipaswa kulipa ili tupate kuachiliwa. Katika kuona serikali ya CCP ikitenda kama waporaji fidhuli na wasio na busara ambao waliwavua watu uhuru wa dini, nilihisi chuki kubwa na sikuweza kujizuia kufikiria maneno ya Mungu: “Kwa maelfu ya miaka hii imekuwa ni nchi ya uchafu, ni chafu sana, shida zimejaa, mizimu wanazunguka kila kona, wakihadaa na kudanganya, wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi[a], wakiwa katili na waovu, wakikandamiza mji huu ulio mahame na kuuacha ukiwa umetapakaa maiti; harufu ya uozo inaijaza nchi na kuenea hewani, na inalindwa isivyo kawaida[b]. Nani awezaye kuuona ulimwengu kupita anga? … Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!” (“Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Katika mahame haya ya China, chama tawala cha China huangika mabango yakikuza “uhuru wa dini na uhuru wa haki za binadamu,” lakini kwa kweli wao humtesa Mungu bila kizuizi na huwakamata na kuwatesa watu wanaomfuata Mungu. Hawaruhusu watu kumwamini Mungu na kutembea kwa njia sahihi ya maisha; walikuwa na hamu ya kuondosha waumini wote kwa dharuba moja. Hatukuwa tumevunja sheria au kufanya chochote kibaya; yote tuliyofanya yalikuwa ni kushiriki injili ili kuwaruhusu watu kumjua Mungu na kumwabudu Mungu na kuacha maisha yao ya giza na maumivu. Hata hivyo, polisi wa CCP walitaka kutukamata, kutuzuia na kututoza faini, badala ya kujishughulisha na wale watu waovu walioshiriki katika umalaya, mauaji na uchomaji wa mali kwa makusudi, na ulaghai na utapeli; waliwaruhusu hawa watu waovu kuepuka adhabu. Kwa sababu ya ukweli huu, niliweza kuona kwamba serikali ya CCP ilikuwa kikundi cha pepo ambacho kilimpinga Mungu, kilichowapofusha na kuwadanganya watu; walikuwa ni adui wa Mungu.

Mnamo Novemba 28 ya mwaka huo huo, ndugu kadhaa wa kiume na wa kike nami tulikuwa tukishiriki injili na kiongozi mmoja wa dini. Lakini tuliripotiwa na mtu muovu na polisi takribani dazeni moja walizungukwa jengo letu na kuvunja kupitia mlango. Walikuwa na bunduki na virungu mikononi mwao na walisema kwa sauti kubwa: “Mtu yeyote asisogee! Wekeni mikono yenu juu!” Waliipekua miili yetu na kuiba fedha zetu na vitu vya thamani vyenye thamani ya zaidi ya yuan 5,000. Walituamuru tuweke mikono yetu juu ya vichwa vyetu na kuchuchumaa tukikabiliana na ukuta. Dada wawili vijana wakati huo waliogopa na nikawaambia: “Hatujafanya chochote kibaya, msiogope.” Mara tu niliposema hayo, polisi kadhaa mara moja walinivamia na kunipiga ngumi na mateke, wakiniangusha sakafuni. Waligeuza vyumba vyote shaghalabaghala na kuvipindua kuwa machafuko. Walikuwa wakatili na wakali zaidi kuliko majambazi wakipora kijiji. Dada mmoja katika chumba hakutoka nje na polisi mmoja mwovu akakurupua na kumshika kwa nguvu na kumvuta nje. Polisi mwingine muovu akaona kwamba alikuwa wa kupendeza sana na akaanza kumsumbua kwa kumugusagusa mwili wake wote. Huyo dada alilia kwa sauti na kwa bahati nzuri mwenye nyumba akafika tu wakati ufaao kukomesha hayo, jambo lililomruhusu huyo dada kuepuka shurutisho hilo. Kwa wakati huu niliweza kuona wazi kwamba miito kama “polisi wa umma wako kwa sababu ya watu na kama una shida yoyote, waite polisi” na “polisi ni waangalizi wa watu” ilikuwa yote ni uongo. Polisi hawa waovu walikuwa tu kundi la wahuni na majambazi wa mahali palepale! Baadaye, walitufungia katika gari la polisi na kutupeleka kwa kituo cha polisi. Kisha walitufunga pingu kwa ushoroba kwa muda wa siku mbili usiku na mchana wakikosa kutupa chochote cha kula au kunywa. Niliweza tu kuomba moyoni mwangu na kumuuliza Mungu atuongoze na kutupa imani na nguvu ili tuweze kuwa mashahidi katika mazingira haya. Baadaye, hao polisi waovu walimhoji ndugu mmoja wa kiume, na wakati wao walipokosa kuridhika na majibu yake, polisi wachache waovu walimsukuma chini sakafuni kwa uthabiti huku polisi mwingine muovu akishindilia kinyesi cha mbwa katika kinywa chake. Hali ya akili ya ndugu huyu ilikuwa imechochewa mno. Kwa kuona hali hii yenye taabu, moyo wangu ukahuzunika mno na ghadhabu ikawaka ndani yangu. Nilitamani kuwa ningeshambulia na kuwararua vipande vipande, lakini neno la Mungu liliuongoza moyo wangu: “Nahisi huruma kidogo kwa ndugu Zangu wanaoishi pia katika nchi hii ya uchafu, kwa hiyo nimekuza chuki kwa joka kuu jekundu. … Sisi sote ni waathiriwa. Kwa sababu hii, Nalichukia kutoka kwa kiini Changu na Siwezi kungoja kuliharibu. Kwa hali yoyote, Ninapofikiria tena, hili halingekuwa na mafanikio na lingeleta tu tatizo kwa Mungu, kwa hiyo Narudi kwa maneno haya—Nimeamua kuyafanya Mapenzi Yake—kumpenda Mungu. … kwa hivyo kuishi kwa kudhihirisha maisha yaliyojaa maana na mng’aro, Nitaweza kufa bila majuto, na moyo uliojaa furaha na faraja. Je, ungependa kufanya hilo? Wewe ni mtu aliye na aina hiyo ya azimio?” (“Njia … (2)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Neno la Mungu lilinisababisha kutulia, na katika kujaribu kulielewa neno la Mungu, nilielewa mapenzi ya Mungu. Mungu tayari anawadharau mashetani hawa waovu, Anatamani kuwaangamiza wote mara moja, lakini ili kukamilisha kazi ya Mungu ya siku za mwisho na kutukamilisha, Yeye anahitaji kutumia juhudi za Shetani. Mungu hutumia mateso yake ili kutuwezesha kumtambua, na hivyo akituwezesha kuona kabisa uso wa kukirihi na tabia ya pepo ya serikali ya CCP. Kwa sababu hiyo tunaweza kumtelekeza na kuvunja uhusiano naye na kuigeuza kabisa mioyo yetu miaminifu kwa Mungu. Mungu daima anavumilia ukimbizaji wenye wayowayo wa CCP ili kupata matokeo mazuri katika kazi Yake, hivyo ni kitu gani kuwa ninapaswa kupitia shida kidogo ili niweze kupata wokovu kama sehemu ya uumbaji? Mungu amenipa nuru na kunipa imani na nguvu; ninataka kumuiga Kristo na kuazimia kwa uthabiti kutekeleza mapenzi ya Mungu—kutafuta kumpenda Mungu! Wakati huu nilitamani tu kwamba Mungu atuongoze na kutuhifadhi ili kuwa shahidi kwa Mungu kupitia mateso hayo ya Shetani; nilipenda kwamba tungeweza kutumia upendo wetu kwa Mungu ili kukabiliana na hila za Shetani ili aweze kushindwa kwa aibu.

Mnamo usiku wa tatu, wale polisi waovu walituhamishia Ofisi ya Usalama wa Umma ya Wilaya na kutuhoji usiku kucha. Naibu mkurugenzi mmoja kwanza alitumia maneno ya kujipendekeza ili kunishawishi, akisema: “Zungumza! Una mke, watoto, na wazazi nyumbani ambao wanahitaji uwatunze; ukifanya haraka na kuzungumza, basi unaweza kwenda nyumbani, sawa?” Baada ya kusikia maneno hayo, nilivutiwa kiasi, na nikafikiri: “Kama nitawaambia vitu fulani visivyo na maana, basi ninaweza kwenda na sitalazimika kukaa hapa na kuteseka.” Wakati huo, nilizinduliwa na maneno ya Mungu: “Sitawahurumia tena wale ambao hawakuwa waaminifu Kwangu kabisa wakati wa majonzi, kwa sababu huruma Yangu ina mipaka. Zaidi ya hayo, Simpendi yeyote yule ambaye amewahi kunisaliti Mimi, wala Sipendi kujihusisha na wale ambao hawawajali wenzao. Bila kujali huyo mtu ni nani, hii ndiyo tabia Yangu” (“Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kupitia maneno ya adhimu ya Mungu, ilikuwa ni kama niliweza kumwona Mungu akinikazia macho chini, akisubiri nimjibu. Kwa hiyo, niliondoa wazo hilo haraka na kwa ukali wa haki nikasema: “Sijapanga kuondoka tangu nilipokuja hapa!” Wakati huyo polisi muovu alipoona kwamba hila yake haikuwa ikifanya kazi, alifichua tabia yake asili ya pepo, na yule naibu mkurugenzi akainua ndoo ya kinyesi cha nguruwe juu ya kichwa changu kama aliyetaka kunimwagilia. Nikamwambia: “Hii ni adhabu ya ukatili na isiyo ya kawaida unayotumia kughusubu ungamo.” Aliposikia nikisema hivi, alisitisha ghafla na kuweka kile kinyesi chini bila kunimwagilia. Polisi mwingine muovu aliyekuwa amevaa viatu vya ngozi alinikanyaga kidole kikubwa cha mguu kwa kisigino chake na kukikunja pande zote kuzunguka kwa shinikizo kubwa kadri alivyoweza. Maumivu makali yalisambaa kotekote mwili wangu mzima na sikuweza kujizuia kulia kwa maumivu. Nguo zilizokuwa mwilini mwangu zililowa kwa jasho, lakini yule polisi muovu alifoka kwa ghadhabu na akaendelea kunikanyaga na kukunja mpaka kidole changu kikubwa cha mguu kikararuka na kulegea. Kufikia wakati huu, kidole changu kilikuwa tayari kimeharibiwa na chenye damu. Katika maumivu yangu makubwa mno, niliendelea kumlilia Mungu, nikimwomba Mungu kuulinda moyo wangu ili nisiweze kukubali kushindwa na Shetani na ili niweze kuwa shahidi Kwake. Ukatili wa shetani ni mwingi zaidi kuliko huu; nilimwona ndugu mmoja akirudi kutoka kwa mahojiano na tayari alikuwa ametiwa maumivu makali kiasi kwamba alikaribia kifo; mwili wake wote ulikuwa umetiwa makovu na kuviliwa na alionekana kama alikuwa akifa. Wale polisi waovu walihofia kwamba angekufa, kwa hiyo walimwachilia shingo upande. Baadaye, walinipeleka pamoja na ndugu mmoja wa kiume na mmoja wa kike kwa kikosi aali cha usalama cha mji huo cha SWAT ili kuhojiwa zaidi.

Tulipofika kwa kikosi cha SWAT, wale polisi waovu walitulazimisha kuvua nguo zetu zote na kisha wakafunga mikono yetu pingu na kuzungusha silisili kwa miguu yetu. Halafu walitulazimisha kurukaruka mizunguko mitatu kuzunguka uga ili kutufedhehesha. Baadaye, walitutenganisha ndani ya seli za gereza. Watu waliofungiwa katika seli za gereza wote walikuwa wauaji, wote walikuwa kama pepo na madubwana. Wale polisi waovu wakawaagiza wafungwa kunitesa, lakini kwa sababu ya ulinzi wa Mungu, hao wafungwa hawakukosa tu kunidhulumu, lakini kwa kweli walinitunza. Baada ya siku nne, hao polisi waovu walijaribu kunilazimisha kumsaliti Mungu na kuwasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike, lakini singezungumza. Walinichukua pamoja na ndugu mwingine na wakatuvuta ndani ya uga ambako walitufunga pingu mikononi na kuizungusha minyororo kwa miguu yetu. Mifuko myeusi iliwekwa juu ya vichwa vyetu na wakatuning’iniza kutoka kwa mti katikati ya uga. Kwa kichaa cha ukatili, waliweka siafu kote mtini, ambao kwa uendelevu walitambaa juu ya miili yetu wakituuma. Mateso ya elfu kadhaa za maumo ya siafu yalikuwa sawa na mateso ya elfu nyingi za mishale kupitia moyoni, jambo ambalo lilifanya kifo kionekane cha kuvutia zaidi kuliko kuishi. Niliweza tu kumwomba Mungu kwa uwezo wangu wote kuulinda moyo wangu na roho, ili Angenipa hiari na nguvu katika mateso yangu, akiniruhusu kupinga kumsaliti Mungu. Kwa wakati huu, maneno ya Mungu yalionekana katika mawazo yangu: “ili utukufu Wangu uweze kujaza ulimwengu, watu wote wanapitia taabu ya mwisho kwa ajili Yangu Mimi. Je unaelewa mapenzi Yangu? Haya ndiyo matakwa ya mwisho ambayo Nataka kutoka kwa mwanadamu, ambalo ni kusema, Natumai kwamba watu wote wanaweza kutoa ushuhuda wenye nguvu, unaovuma Kwangu mbele ya joka kubwa jekundu, kwamba waweze kujitolea wenyewe Kwangu kwa mara ya mwisho, na kutimiza matakwa Yangu kwa mara nyingine ya mwisho. Je, nyinyi mnaweza kufanya hili kweli? Nyinyi hamkuweza kuuridhisha moyo Wangu katika siku zilizopita—je, mnaweza kuvunja mpangilio huu katika mara ya mwisho?” (“Sura ya 34” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalisababisha moyo wangu kujazwa na nguvu. Mungu aliteseka kufuatiliwa kwa kila njia zilizowezekana na serikali ya CCP ili kutuokoa. Alikuwa hana mto na hakuwa na mahali pa kuita nyumbani. Leo ninaweza kuteseka na Kristo; huu ni upendo wa Mungu na ni kuinuliwa kwangu na Mungu. Alimradi ninaweza kumtukuza Mungu, nitakuwa na furaha na niko tayari kufa. Nililitegemea neno la Mungu ili kupitia kila dakika na sekunde ya maumivu hayo. Tulining’inizwa juu ya mti huo kwa siku mbili usiku na mchana. Siku ya tatu, sikuweza kustahimili tena. Ilikuwa mapema msimu wa baridi wakati huo na mvua ilikuwa inanyesha na yote niliyovaa ilikuwa ni vazi moja bila bitana. Nilikuwa nimening’inizwa kutoka kwa mti huo kwa miguu yangu mitupu na sikuwa nimepata chochote cha kula au kunywa. Mateso ya njaa na baridi pamoja na maumivu yasiyovumilika yalinifanya nitake kufa; yote niliyoweza kufanya ni kuomba kwa kila njia. Niliogopa kwa kina kwamba kwa sababu ya udhaifu wa mwili, singeweza kuvumilia mateso na ningemsaliti Mungu. Katikati ya maumivu yangu, nikakumbuka mtume Stefano kutoka kwa Enzi ya Neema. Alipigwa kwa mawe hadi kufa na umati kwa sababu alikuwa akieneza injili ya Bwana Yesu. Kabla ya kufa, alimwomba Mungu aikubali roho yake. Kwa hiyo, nikamwomba Mungu: “Ee Mungu, mwili wangu ni dhaifu mno na sasa nimechukua maumivu zaidi ya ninavyoweza kuvumilia. Ninapenda kwamba ungechukua roho yangu, kwa maana afadhali nife kuliko kukusaliti Wewe.” Baada ya kuomba, muujiza usiotarajiwa mno ulifanyika: nilikuwa na uzoefu wa kuwa nje ya mwili na nikaletwa kwa uwanja wa nyasi. Kulikuwa na nyasi ya kusitawi sana, ya kijani kila mahali na ng’ombe na kondoo wakiuzunguka. Hali yangu ya muda ya akili lilikuwa na utulivu hasa na sikuweza kujizuia kumsifu Mungu kwa sauti: “Msifu Mwenyezi Mungu kwa sauti, vitu vyote mbinguni na duniani hukusifu Wewe, hukukusifu Wewe, vyote vitakusifu Wewe. Acha malaika Wako wote wainuke na kukusifu, acha majeshi Yako yote ya mbinguni ikusifu Wewe, mtanuko wa ulimwengu hukusifu Wewe—Mwenyezi Mungu! Nyota zinazoangaza hukusifu Wewe, mbingu na ardhi na maji hukusifu Wewe, vyote hukusifu. Acha milima na vilima vimsifu Mwenyezi Mungu, Acha mawimbi na mawimbi makubwa yakusifu Wewe, yakusifu Wewe katika mahali pa juu mno—Mwenyezi Mungu! Msifu Mwenyezi Mungu katika mahali patakatifu sana, yakusifu Wewe kwa kigoma na ngoma, yakusifu Wewe kwa sauti! Msifu Mwenyezi Mungu kwa vyombo vya muziki na sauti ya tarumbeta, acha watu watakatifu Sayuni wakusifu, acha watu wote wakusifu Wewe—Mwenyezi Mungu! Ee Mwenyezi Mungu, wakusifu Wewe kwa sauti! Ngurumo kubwa za radi hukusifu Wewe, hukukusifu Wewe kwa sauti! Eneo kubwa pana na wazi humsifu Mwenyezi Mungu, acha kila kitu kilicho na pumzi kikusifu Wewe, kuimba kwa sifa hutetemesha miisho ya dunia, Mungu asifiwe!” (“Msifuni Mwenyezi Mungu kwa Sauti Kuu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilipojitosa kabisa katika furaha hii isiyo kifani na kuishi katika mipaka ya uhuru, maumivu, njaa na baridi ya kuning’inizwa kutoka kwa mti na vilevile maumivu ya kuumwa na siafu yote yalitoweka. Nilipoamka, ilikuwa tayari usiku wa tatu na wale polisi waovu walinishusha kutoka kwa mti. Niliangikwa kwa siku tatu na sikukosa tu kufa, pia nilikuwa nimejaa uchangamfu. Hii kwa kweli ilikuwa ni nguvu yenye enzi na ulinzi wa miujiza wa Mungu! Nilitoa shukrani za dhati na sifa kwa Mungu.

Mnamo siku ya nne, wale polisi waovu walinihoji tena na wakajaribu kunilazimisha niwasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike; pia walinilazimisha kukubali kwamba niliamini katika Xie Jiao, kunifanya nimsaliti Mungu na kuiacha njia ya kweli. Nuru ya Mungu ilinifanya nifikirie neno la Mungu: “Wakati wanapitia majaribu, ni kawaida kwa watu kuwa dhaifu, au kuwa na uhasi ndani yao, au kukosa uwazi juu ya mapenzi ya Mungu au njia yao ya kutenda. Lakini katika hali yoyote, lazima uwe na imani katika kazi ya Mungu, na usimkane Mungu, kama Ayubu” (“Ni Lazima Wale Wanaofaa Kukamilishwa Wapitie Usafishaji” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinipa ujasiri wa kuweka ukweli katika matendo na kutoa ushahidi juu ya Mungu. Bila kujali ni nini, sikuweza kumpinga Mungu au kumkufuru Mungu. Kwa hiyo, kwa ujasiri na kwa imani nilisema: “Naamini katika Mwenyezi Mungu, ambaye ndiye Mungu wa pekee wa kweli anayevitawala vitu vyote! Siamini katika Xie Jiao, mnageuza ukweli na kunizulia uongo!” Baada ya polisi mmoja muovu kusikia jambo hili, alikasirika sana na kunyakua stuli moja ndefu ya mbao na akaanza kunipiga nayo kwa mda mrefu kikatili. Alinipiga kiasi kwamba nilikuwa nikitema damu. Nililala nikiwa nimeduwazwa na nimezimishwa sakafuni. Walipoona kwamba nilikuwa nimepoteza fahamu, walinirashia maji baridi ili kuniamsha na kuendelea kunipiga. Wakati wa kupigwa huku kishetani na kinyama, upande wa mbele wa kifua changu na mgongo wangu zilikuwa nyeusi na bluu kabisa na nilipitia madhara mengi ya ndani. Wiki moja baadaye, mkojo wangu ulikuwa wote ni damu na figo yangu ya kulia iliharibiwa kwa sana (hata leo bado ina uchungu sana). Mwezi mmoja baadaye, hao polisi waovu hawakuweza kupata ushahidi wowote, kwa hiyo walibuni vitu vya uongo na kunilazimisha kutia sahihi. Kisha wakanifunga ndani ya kituo cha kizuizi cha jiji. Miezi mitatu baadaye, walinishtaki na “kuharibu utekelezaji wa sheria za kijamii” na kunihukumu mwaka mmoja wa marekebisho kupitia kazi. Kwa kambi ya kazi, niliishi maisha ya kinyama. Kila siku nilikuwa na njaa na nilipaswa kufanya kazi takribani saa kumi na mbili kwa siku. Nilidhulumiwa na kufedheheshwa mara kwa mara na polisi wa gereza; ama walikuwa wanatumia virungu vya umeme au kunifungia ndani ya chumba kidogo, cha giza. Isingekuwa Mungu kunitunza na kunilinda, ningekuwa nimeteswa na hao polisi waovu hadi kifo. Mnamo Novemba 7, mwaka wa 2003, hukumu yangu ilitimizwa na niliachiliwa kutoka kwa hiyo jahannamu ya duniani.

Baada ya kupitia mateso hayo ya ukatili, hatimaye niliona kwa dhahiri kwamba matangazo ya serikali ya CCP “chama cha Kikomunisti ni kizuri, cha utukufu na sahihi” na “China ina uhuru wa dini” kati ya misemo mengine, kwa kweli ni maonyesho tu katika njama mbovu ya kuidanganya umma na kuwapumbaza wananchi. Kwa kweli ninamchukia huyu shetani mzee kwa dhati. Yeye huzungumza maneno ya kujipendekeza na hufanya mambo maovu mno. Ili kupiga marufuku kazi ya Mungu ya siku za mwisho na kufanya China kuwa mahali pa wamkanao Mungu, huwa inafuatilia na kuwaua waumini bila kizuizi. Kiwango chake cha ukatili tayari kimefikia vimo vikubwa na imewafanya watu wapandwe na mori! Ninafikiria nyuma kuhusu jinsi nilivyokuwa nikiteswa kwa ukatili na kulazimishwa kufanya ungamo na kuteswa kwa ukatili na pepo wakati wa mchakato wangu wa kuhojiwa. Niliduwazwa mara kadhaa na kama haingekuwa ulinzi wa Mungu, ningekuwa ningeteswa hadi kufa na pepo hao. Wakati wa udhaifu wangu mkuu, neno la Mwenyezi Mungu lilinitumainisha kwa mfululizo: “Mmewahi kuzikubali baraka mlizopewa? Mmewahi kutatufa ahadi mlizopewa? Hakika, chini ya mwongozo wa mwangaza Wangu, mtapenya utawala wa nguvu za giza. Hakika, katikati ya giza, hamtaupoteza mwangaza unaowaongoza, katikati ya giza. Hakika mtakuwa bwana wa viumbe vyote. Hakika mtakuwa washindi mbele ya Shetani. Hakika, wakati wa maangamizi ya ufalme wa joka kubwa jekundu, mtasimama miongoni mwa umati mkubwa kushuhudia ushindi Wangu. Hakika mtakuwa shujaa na imara katika nchi ya Sinimu. Kupitia mateso mnayoyavumilia, mtarithi baraka zinazotoka Kwangu, hakika mtaangaza ndani ya ulimwengu wote kwa utukufu Wangu” (“Sura ya 19” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili).

Maneno ya Mungu yalinipa kitu imara cha kutegemea! Kiliniruhusu kufurahia nuru na mwongozo wa maneno ya Mungu wakati wa maumivu yangu ya kuzidi kiasi na udhaifu, ambayo ndiyo iliyokuwa njia ya pekee ambayo ningeweza kupita kipindi hiki cha giza na kilichorefuka kupita kiasi Ingawa nimepata uzoefu wa kukamatwa na kuteswa mara nyingi na serikali ya CCP, na mwili wangu umepitia ukatili usio na huruma na mateso, kwa kweli naelewa ukweli mwingi ambao sikuufahamu katika siku za nyuma na ninaona kwa dhahiri tabia ya kishetani ya uovu unaopinga maendeleo wa serikali China. Nimepata uzoefu pia wa upendo wa kweli wa Mwenyezi Mungu kwangu na nimeonja hekima inayoweza ya Mwenyezi Mungu na matendo ya ajabu. Huniamsha kutafuta kumpenda Mungu na kumridhisha Mungu. Leo, bado ninatimiza wajibu wangu katika kanisa kama nilivyofanya zamani; mimi humfuata Mungu katika njia sahihi ya uzima, mimi hutafuta ukweli na hutafuta kuishi maisha ya maana.

Tanbihi:

a. “Wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi” inahusu mbinu ambazo ibilisi hutumia huwadhuru watu.

b. “Inalindwa isivyo kawaida” inaonyesha kuwa mbinu ambazo ibilisi hutumia huwatesa watu ni mbovu hasa, na kuwadhibiti watu sana kiasi kwamba hawana nafasi ya kusogea.

Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu

 

Views: 116 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: Maneno ya Mungu, mapenzi ya Mungu, Enzi ya Neema | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar