Mwenyezi Mungu anasema, Sauti Yangu inatoka kama radi, ikitia nuru roboduara zote nne na dunia nzima, na katikati ya radi na umeme, binadamu wanaangushwa chini. Hakuna mwanadamu aliyewahi kusimama imara katikati ya radi na umeme: Wanadamu wengi wanaogopa sana kuja kwa mwangaza Wangu na hawajui cha kufanya. Wakati mwangaza hafifu unaanza kuonekana Mashariki, watu wengi, wakiongozwa na huu mng’ao dhaifu, wanaamshwa mara moja kutoka kwa njozi zao. Lakini, hakuna aliyewahi kutambua kwamba siku imewadia mwangaza Wangu unaposhuka duniani. Wanadamu wengi wanashtuliwa na ujio wa ghafla wa mwangaza; baadhi yao, kwa macho ya kuvutiwa ya dadisi, wanaangalia mwendo wa mwanga ... Read more »

Views: 136 | Added by: flickrpinquorettfb | Date: 05.24.2019 | Comments (0)