Kufuata kuanza kazi kwa mtazamo mpya, kutakuwa na hatua mpya katika kazi Yangu. Kama ilivyo katika ufalme, Nitafanya mambo moja kwa moja kupitia kwa uungu, Nikiongoza kila hatua ya njia, sahihi hadi kwa maelezo madogo, na bila kutiwa najisi na nia za binadamu hata kidogo. Yafuatayo yanaeleza kwa muhtasari namna ya utekelezaji halisi: Kwa vile ni kupitia katika ugumu na usafishaji ndiyo wamepata jina la “watu”, na kama walivyo watu wa ufalme Wangu, lazima Niwafanye watii kwa mahitaji kali, ambayo ni ya juu kushinda mbinu za kazi Yangu kwa vizazi vilivyopita. Huu sio tu uhalisi wa maneno, bali pia la muhimu zaidi ni uhalisi wa kutenda, na hili lazima kwanza litimizwe. Katika kila neno na matendo, ni lazima watosheleze viwango vinachohitajika kwa watu wa ufalme, na mkosaji yeyote ataondolewa mara moja, ili kuzuia aibu k
...
Read more »