Yohana alimfanyia Yesu kazi kwa miaka saba, na tayari alikuwa ameandaa njia Yesu alipofika. Kabla ya haya, injili ya ufalme wa mbinguni iliyohubiriwa na Yohana ilisikika kotekote katika nchi, hivyo ilienea kutoka upande mmoja hadi upande mwingine wa Uyahudi, na kila mtu alimwita nabii. Wakati huo, Mfalme Herode alitamani kumuua Yohana, lakini hakuthubutu, kwani watu walimheshimu sana Yohana, na Herode aliogopa kwamba kama angemuua Yohana wangemuasi. Kazi iliyofanywa na Yohana ilikita mizizi miongoni mwa watu wa kawaida, na aliwafanya Wayahudi kuwa waumini. Kwa miaka saba alimwandalia Yesu njia, mpaka wakati ambapo Yesu alianza kutekeleza huduma Yake. Na kwa hiyo, Yohana alikuwa mkuu zaidi kwa manabii wote. Yesu alianza tu kazi Yake rasmi baada ya Yohana kufungwa jela. Kabla ya Yohana, hakukuwahi kuwa na nabii aliyemwandalia Mungu njia, kwa sababu ka ... Read more »

Views: 102 | Added by: flickrpinquorettfb | Date: 01.03.2020 | Comments (0)