7:24 PM
Ushuhuda wa Maisha | Nilijifunza Kufanya Kazi na Wengine

Liu Heng Mkoa wa Jiangxi

Kupitia neema ya Mungu, nilichukua jukumu la kuwa kiongozi wa kanisa. Wakati huo, nilikuwa na shauku mno na niliweka azimio mbele ya Mungu: Bila kujali kinachonikabili, sitayatelekeza majukumu yangu. Nitafanya kazi vizuri na yule dada mwingine na nitakuwa mtu anayetafuta ukweli. Lakini nilikuwa nimeamua tu, na sikujua jinsi ya kuingia katika uhalisi wa uhusiano wa kufanya kazi kwa mpangilio wa kuridhisha. Nilipoanza kwanza kupanga masuala ya kanisa na dada ambaye nilikuwa nikifanya kazi naye, na tulipokuwa na maoni tofauti, ningemwomba Mungu kwa uwazi nikimuuliza Yeye kuulinda moyo wangu na roho yangu ili nisimlaumu mshirika wangu. Hata hivyo, nilizingatia tu kudhibiti vitendo vyangu ili nisiwe na migogoro na mshirika wangu, kwa hivyo sikuwa nimeingia katika ukweli. Kwa hiyo, baada ya muda, nilikuwa na kutoafikiana zaidi na zaidi na dada huyu. Wakati mmoja nilitaka kumpandisha cheo dada mmoja ili achukue wajibu wa kuwanyunyiza waumini wapya na dada niliyekuwa nikifanya kazi naye alisema kuwa dada huyo hakuwa wa kufaa. Baada ya kumbadilisha mteuliwa wangu, bado alisema hakuwa anafaa. Nilikasirika kwa haraka na kwa hasira nikasema: “Hakuna mtu anayefaa, ni wewe tu unayefaa!” Kwa hiyo, sikuwahi kuzua jambo hilo tena. Alipouliza kuhusu hilo, nikasema kwa ghadhabu: “Chagua yeyote unayemtaka! Sijali!” Baada ya hilo, bila kujali kile alichokisema, kama kulikuwa na ugomvi wowote, singesema chochote, ningelishikilia ndani nikifikiri kwamba ningeweza kwa hivyo kuepuka ugomvi. Wakati mwingine kulishikilia ndani kukawa hakuvumiliki, kwa hiyo ningejificha mahali fulani na kulia, nikihisi kwamba nilikuwa nimekosewa. Na hata nikawaza: Si wewe una uwezo? Basi lifanye mwenyewe! Nitatazama ukijifanya kuwa mpumbavu! Wakati mmoja baadaye, Kiongozi wa ngazi ya juu alinipa kazi fulani ya kushughulikia. Jambo lote liliamuliwa na kupangwa na mimi mwenyewe, na nilihisi kuridhika kabisa na jambo hilo. Nilidhani dada niliyekuwa nikifanya kazi naye angenisifu na kunifariji. Bila kutarajia, mshiriki wangu akakikataa kama kwamba sufuria ya maji baridi yalikuwa yakimiminwa juu yangu, akisema: “Hii kweli siyo njia sahihi ya kufanya hili.” Hili kwa kweli lilinikasirisha sana. Niliwaza: Hata hukuelewa hali halisi na umeikataa katakata. Hayo kwa kweli ni majivuno! Kwa hiyo, kila mmoja wetu alishikilia maoni yake na hakuna yeyote aliyekuwa tayari kumnyenyekea mwenzake. Baadaye, singesikiliza hata mawasiliano ya neno la Mungu. Jinsi niliyozidi kuliwazia, ndivyo niliyozidi kuhisi kuwa alikuwa na makosa. Alikuwa ni yeye aliyetumia ukubwa wake kwa makusudi kupata manufaa kwa kufanya mambo yawe magumu kwangu. Nilifikiria pia jinsi nilivyomvumilia mara kwa mara, lakini bado alinitendea kwa njia hii. … Jinsi nilivyozidi kulifikiria ndivyo nilivyozidi kuhisi nilikosewa, mpaka nilipoachwa kabisa katika giza na nilikuwa nimepoteza kazi ya Roho Mtakatifu. Kuanzia wakati huo kwendelea, sikuwa tayari kufanya kazi naye. Niliwaza: Kwa kuwa ni vigumu kulishughulikia, nitajifichia kutoka hilo tu. Wakati huo nilifahamu pia kwamba hali ya aina hii ilikuwa hatari mno. Nilifikiria ingekuwa bora kuomba nibadilishiwe wajibu haraka iwezekanavyo ili kuepuka kufanya kitu kibaya. Kwa hiyo, nilitumia kimo changu kidogo na kutoweza kwangu kama kisingizio cha kuandika barua yangu ya kujiuzulu. Muda mfupi baadaye, kiongozi wa ngazi ya juu akawasiliana kwangu kuhusu kanuni ya kukubali kushindwa na kujiuzulu na pia nadhari kubwa ambayo Mungu ameweka katika kuwaokoa watu. Lakini nilikuwa nimeufanya moyo wangu kuwa mgumu na haungekuwa mwororo.

Asubuhi iliyofuata baada ya kuondoka kitandani, kichwa changu kilikuwa kitupu kabisa. Hata nilipoomba, singeweza kumhisi Mungu na nikahisi kana kwamba Mungu alikuwa ameniacha. Niliogopa na kuhangaika; bila shaka ulikuwa ni mwenendo wangu uliomfanya Mungu kunichukia. Kwa hiyo nilianza kujichunguza. Baada ya kufikiria kila kitu kilichokua kimetokea, niliweza kuona kwamba tabia yangu ilimfanya Mungu kunichukia. Mawazo yangu na matendo yangu yalikuwa sawa kabisa na ya mtu asiyeamini. Niliishi kama mtu asiyeamini Mungu, ambaye alisalia bila kubadilika. Neno la Mungu halikuwa katika mwenendo wangu na sikuwa namcha Mungu. Sikuwa mtu aliyekubali ukweli kabisa. Kwa sababu hiyo, nilikuwa nimedanganywa na Shetani na nilikuwa nimesalimisha majukumu yangu bila kujua. Baada ya kufahamu jambo hili, mara moja nilijishusha mbele ya Mungu na kutubu: “Ee Mwenyezi Mungu, nimekosa. Nimekwamini Wewe, lakini sijakuwa radhi kupitia kazi Yako. Ulipanga mazingira yangu na sijakuwa nikiridhia kulikubali; nilitaka kuepuka adhabu na hukumu yako kikamilifu, na wakati upendo Wako ulipokuja kwangu, sikukosa tu kutoa shukrani, pia nililalamika Kwako na kukuelewa Wewe visivyo. Mwenendo wangu umekuumiza Wewe. Ee Mungu, nakushukuru kwa kunifichua katika kazi Yako na kuniruhusu kutambua tabia ya Shetani iliyo ndani yangu. Kama haingekuwa hivyo, bado ningedhani kwamba sikuwa mbaya. Sasa naona kwamba kimo changu kwa hakika ni kidogo sana. Siwezi kushughulikia hata vipingamizi vidogo zaidi. Wakati kitu chochote kidogo ambacho sikipendi kinatokea, nataka kukusaliti. Nimeziacha viapo nilivyoweka na Wewe. Ee Mungu, niko tayari kutubu; niko tayari kujijua kupitia maneno Yako na kukubali hukumu na kuadibu kwa maneno Yako. Niko tayari kujiweka chini kwako katika mazingira haya na kufanya kazi vizuri na huyu dada. Ee Mungu, siko tayari tena kuishi chini ya miliki ya Shetani na kuzuiliwa na tabia yangu potovu. Siko tayari tena kuishi kwa sababu ya hadhi yangu mwenyewe, lakini niko tayari kukuridhisha Wewe mara moja!” Baada ya kuomba, nilitokwa na machozi na punde baadaye nilifuta barua yangu ya kujiuzulu na kuichana vipande vipande papo hapo. Tulipokusanyika siku hiyo, wachache wetu tulikuwa tukilisoma neno la Mungu pamoja: “Sifa zenu tayari zimeharibiwa, mwenendo wenu unashuka hadhi, njia yenu ya kuzungumza ni ya chini, maisha yenu ni ya kudharauliwa, na hata ubinadamu wenu wote ni wa chini. Nyinyi ni wa mawazo finyu kwa watu na nyinyi hubishana juu ya kila kitu kidogo. Nyinyi hugombana juu ya sifa zenu na hadhi zenu wenyewe, hata kufikia kiasi kwamba mko radhi kushuka kuzimu, katika ziwa la moto” (“Tabia Yako Ni Duni Sana!” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Watu huwa hawadai mengi kutoka kwao wenyewe, lakini hudai mengi kutoka kwa Mungu. Wanamtaka Mungu kuwatunukia hasa, na kuwa na subira na uvumilivu kwao, kuwatunza, kuwaruzuku, kuwatabasamia, kuwatunza kwa njia nyingi, na kwamba Hawezi kuwa mkali kwao hata iweje wala kufanya chochote ambacho kinawakasirisha hata kidogo, lakini Anaweza kuwabembeleza tu kila siku. Mantiki ya mtu ina upungufu sana!” (“Watu Ambao Daima Wana Mahitaji kwa Mungu Ndio wa Mwisho Kuwa Tayari Kusikia Hoja” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Neno la Mungu lilikuwa limefunua kabisa hali yangu ya kutahayarisha na sura mithili ya shetani. Nilikuwa na aibu sana kiasi kwamba sikuweza kujizuia kutamani mwanya uwe ardhini ili niweze kutambaa ndani. Kupitia ufunuo na kupata nuru kwa neno la Mungu, niliweza kuona kwamba tabia ya Shetani ndani yangu ilikuwa kubwa sana. Nilikuwa na asili ya kiburi na majivuno mno kiasi kwamba nilihisi kuwa nilikuwa bora kuliko watu wengine. Sikuwa na kiasi hata kidogo cha kujitambua; sikuelewa kwamba sikuwa bora. Kwa hiyo, nilipokuwa nikifanya kazi na yule dada, daima nilidhani kwamba nilikuwa msimamizi, kwamba nilikuwa kiongozi. Nilikuwa na hamu ya dada kunifuata katika kila kitu na kunisikiliza. Daima nilidhani kwamba nilikuwa kiongozi. Wakati maoni ya dada yalipingana na yangu mwenyewe, sikutafuta ukweli kutatua mgogoro au kufikia mapatano ya pamoja. Badala yake, ningepandwa na hasira na kutwaa mtazamo kwa sababu nilikuwa nimeona aibu kiasi kwamba ningeacha kazi yangu ili kutoa nje kukata tamaa kwangu. Nilikuza mawazo kabla ya kujua ya huyu dada na kamwe sikuchukua hatua ya kwanza kuboresha uhusiano wetu mbaya. Tulipokuwa tukifanya kazi pamoja, daima ningeonyesha mtazamo ulio karimu. Sikujihitaji kubadilika, nilidharau kuzungumza kwa dhati na huyu dada . Ningemlenga yeye na kumhitaji ajibadili. Nilijiona kuwa bwana wa ukweli na kuwaona watu wengine kama wapotovu. Wakati wote wa mchakato wa kufanya kazi pamoja, sikujichunguza. Wakati dada alikuwa na mtazamo mbaya, au wakati kulipokuwa na tofauti ya maoni kati yetu, basi ningechukua lawama yote na kuiweka kwa mshiriki wangu. Niliamini kwamba alikuwa na kosa nami nilikuwa sahihi, hivyo nilimdunisha katika moyo wangu na kumbagua kiasi kwamba nilimchukua kama tu adui, nikitaka kumwona mshiriki wangu ajifanye mpumbavu. Katika kuona kiburi changu, majivuno ya kishenzi, upumbavu, na tabia yangu ya kustahili kushutumiwa kabisa, na vilevile tabia yangu ya wawazo finyu, kungekuwaje na hisi ya kawaida ya ubinadamu iliyobaki ndani yangu? Kwa hakika nilikuwa muhali! Mungu alinipa neema Yake na kunipa fursa ya kuchukua jukumu, lakini sikufikiria kuhusu kufanya kazi vizuri na huyu dada katika kazi zetu ili kumridhisha Mungu. Siku nzima, singejihusisha na kazi nyofu, ningefanya hila dhidi yake, na ningekuwa na migogoro ya wivu naye. Siku nzima nilijua tu kubishanabishana juu ya malalamiko yangu mwenyewe na kwa mfululizo kupigania hadhi yangu mwenyewe na mambo yasiyofaa. Je, nilikuwa na dhamiri ya busara? Je, nilikuwa mtu ambaye alitafuta ukweli? Tangu mwanzo, huyu dada na mimi hatukunyenyekeana wala kuungana mkono katika kazi yetu; badala yake, tulitwaa madaraka sisi wenyewe na kufanya mambo sisi wenyewe. Je, si nilikuwa kwa njia ya mpinga Kristo? Si kufanya mambo jinsi hii kulikuwa kunaelekea kwa kujiangamiza mwenyewe? Leo, ninaweza kuona kwamba mwenendo wangu wote ulikuwa juu ya tamaa za ubinafsi za mwili. Asili yangu ilikuwa yenye ubinafsi mno na yenye kusikitisha. Sikufuatilia ukweli hadi kiasi kwamba miaka yangu mingi ya kumwamini Mungu haikuniletea chochote halisi na hapakuwa na chembe ya mabadiliko katika tabia yangu. Mungu hututaka kuweka neno Lake katika matendo maishani mwetu, lakini mimi hujiondoa kutoka kwalo katika kutimiza majukumu yangu. Mimi kweli ni mtu asiyeamini! Sikuweza kuendelea jinsi hii, nilikuwa tayari kutafuta ukweli na kujibadilisha.

Baadaye, nilisoma neno la Mungu likisema: “Ikiwa ninyi watu ambao mnaratibu kufanya kazi katika makanisa hamjifunzi kutoka kwa kila mmoja, na kuwasiliana, kufidia mapungufu ya kila mmoja, mnaweza kujifunza masomo kutoka wapi? Mnapokutana na chochote, mnapaswa kushirikiana na kila mmoja, ili maisha yenu yaweze kufaidika. … Lazima mfikie ushirikiano wa upatanifu kwa kusudi la kazi ya Mungu, kwa manufaa ya kanisa, na kwa kuwachochea ndugu na dada kuendelea. Unashirikiana pamoja naye na anashirikiana na wewe, kila mmoja akimbadilisha mwingine, mkifikia matokeo bora ya kazi, ili kutunza mapenzi ya Mungu. Huu tu ndio ushirikiano wa kweli, na watu kama hao tu ndio wana kuingia kwa kweli. … Kila mmoja wenu, kama watu wanaohudumu, lazima muweze kulinda maslahi ya kanisa katika yote mnayofanya, badala ya kuwa macho kwa maslahi yako mwenyewe. Haikubaliki kufanya pekee yako, pale ambapo unamdharau naye anakudharau. Watu wanaotenda kwa njia hii hawafai kumhudumia Mungu!” (“Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya” katika Neno Laonekana katika Mwili). Ilisemwa katika mahubiri: “Hakuna wajibu mkuu na naibu wakati wa kuhudumu katika kuratibu. Kila mtu yuko mahali sawa, na kanuni ni kufikia makubaliano kupitia kushiriki kuhusu ukweli. Hili huhitaji kila mtu atii mwingine. Yaani, yeyote anayezungumza kwa usahihi na anazungumza kwa namna inayokubaliana na ukweli anapaswa kutiiwa. Kanuni ni kutii ukweli. Ukweli ni mamlaka, na yeyote anayeweza kushiriki kuhusu kitu kinachoambatana na ukweli na aone vitu kwa usahihi anapaswa kutiiwa. Bila kujali kile watu hufanya au ni wajibu gani wanakamilisha, kutii ukweli daima ni kanuni” (“Maana na Maelezo ya Kanuni Kumi za Maisha ya Kanisa na Familia ya Mungu” katika Kumbukumbu Zilizochaguliwa za Kihistoria za Mipangilio ya Kazi ya Kanisa la Mwenyezi Mungu). Kutokana na ushirika na neno la Mungu, niliona jinsi uratibu katika huduma unavyopaswa kutiwa katika vitendo. Yaani, kufikiria mapenzi ya Mungu na kulinda maslahi ya familia ya Mungu wakati wa kufanya kazi pamoja. Bila kujali ni nini kinachofanywa au kazi ni gani, ni lazima yote ifanywe kwa kunyenyekea ukweli kwa kuwasiliana ukweli ili kufikia mapatano ya pamoja. Huwezi kuwa na kiburi na majivuno sana kiasi cha kudumisha maoni yako na kuwafanya wengine wakusikilize, na huwezi kuuza ukweli ili kulinda uhusiano wako ya watu wawili. Aidha, huwezi kuufuata ubinafsi ili kusababisha uhuru, unapaswa kunyenyekea na kuchukua hatua ya kwanza kujinyima, kujifunza kutoka kwa nyinyi kwa nyinyi, na kufidia udhaifu wa nyinyi kwa nyinyi ili kupata uhusiano wa kufanya kazi wenye kuridhisha. Ni kwa kuingia tu katika aina hii ya uhusiano wa kweli wa kufanya kazi, kumridhisha Mungu katika kila kitu na moyo mmoja na akili moja, na kufidia udhaifu wa nyinyi kwa nyinyi ndipo mnaweza kuwa na baraka za Mungu na mwongozo, na hivyo kuruhusu kanisa kufikia matokeo bora katika kazi yake huku pia mkinufaisha maisha yenu wenyewe. Kwa kinyume, kama wewe ni mwenye kujigamba wakati mnapofanya kazi pamoja, kama hutafuti kanuni ya kweli na kufanya udikteta kuwadhibiti wengine, au kama unafanya kazi peke yako na kujitegemea kufanya mambo, basi utapatwa na chuki ya Mungu na kusababisha hasara kwa kanisa la Mungu. Hata hivyo nilikuwa na kiburi na daima nilitaka kuwa na uamuzi wa mwisho. Nilijuaje kwamba kazi katika familia ya Mungu haikuwa kitu ambacho mtu mmoja angeweza kufanikisha? Watu wote hawana ukweli na wamepungukiwa mno. Kujitegemea kufanya kitu husababisha ajali ziwe na uwezekano mkubwa wa kutokea. Ni kwa njia ya kazi ya kushirikiana tu kazi zaidi ya Roho Mtakatifu inavyoweza kupatikana ili kufidia upungufu wetu na kuzuia makosa. Wakati huo, sikuweza kujizuia kuhisi mwenye hatia na wa kujilaumu kwa tabia ya Shetani ambayo ilifichuliwa katika ujinga wangu na ubinafsi, na kwa kutokuwa hata na chembe ya nadhari kwa mapenzi ya Mungu, na vilevile kwa kuzingatia tu kuepuka aibu kiasi cha kuonyesha tabia ya kushtua na fidhuli. Ninaamini kwamba nilikuwa kipofu sana na mpumbavu, na sikuielewa nia ya Mungu ya kupanga mazingira kwa ajili yangu kutenda ushirikiano katika huduma—hata kwa kiasi kwamba sikuwa na ufahamu hata kidogo wa jinsi ya kujifunza kutoka kwa uwezo za mshirika wangu kufidia upungufu wangu, au jinsi ya kujifunza kile nilichohitaji kupitia kufanya kazi pamoja. Kama matokeo, limesababisha hasara kwa kanisa na kuchelewesha ukuaji wangu mwenyewe katika maisha. Leo, bila huruma ya Mungu na bila mwanga wa neno la Mungu, singeweza kujiachilia na singejua kwamba sikuwa bora zaidi. Bado ningetaka wengine kunisikiliza, kana kwamba ningeweza kujitegemea mwenyewe kufanya kazi ya kanisa vizuri. Mwishowe, ni nani anayejua ni maafa gani yangeibuka? Kwa hiyo, nimeweka azimio: Niko tayari kutenda kulingana na neno la Mungu, niko tayari kufanya kazi kwa mpangilio wa kuridhisha na huyu dada kwa ajili ya kazi ya kanisa na kwa ukuaji wangu katika maisha na sitayafikiria maslahi yangu tena.

Baadaye, nilijiweka wazi kwa dada niliyekuwa nikifanya kazi naye kuhusu jinsi nilivyojijua. Kwa hakika tuliwasiliana na kuingia kanuni ya kuhudumu pamoja. Ambapo baadaye, kazi yetu ilikuwa na mpangilio wa kuridhisha zaidi. Wakati tulipokuwa na maoni tofauti, tuliomba kwa ajili ya ukweli na tukatafuta mapenzi ya Mungu. Tulipoona dosari za sisi kwa sisi, tulikuwa wenye kuelewa hisia za wengine na wenye huruma; tulitendeana kwa upendo. Pasipo kujua, tulihisi baraka za Mungu na matunda ya kazi ya injili zilifichuliwa zaidi kuliko zamani. Wakati huu niliichukia hata zaidi asili ya upotovu niliyokuwa nayo; nilichukia kwamba sikutafuta ukweli na nilikuwa nimemsikitisha Mungu mno. Hatimaye nilipitia ladha nzuri ya kuweka ukweli katika vitendo na nimehisi nguvu zaidi ya kutimiza majukumu yangu na kuufariji moyo wa Mungu. Kuanzia sasa na kwendelea niko tayari kuingia katika uhalisi wa vipengele zaidi vya ukweli na kutafuta kuwa na kanuni katika kila kitu ninachokifanya.

Chanzo:  Ushuhuda wa Maisha | Nilijifunza Kufanya Kazi na Wengine

Views: 126 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: mapenzi ya Mungu, Kanisa, neno la Mungu, ukweli | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar