8:50 PM
38. Maana Halisi ya Uasi Dhidi ya Mungu

38. Maana Halisi ya Uasi Dhidi ya Mungu

Zhang Jun Mji wa Shenyang, Mkoa wa Liaoning

Katika siku za nyuma, niliamini kuwa “uasi dhidi ya Mungu” ilimaanisha kumsaliti Mungu, kuacha kanisa, au kuutelekeza wajibu wa mtu. Nilidhani tabia hizi hufanyiza uasi. Kwa hiyo, wakati wowote niliposikia kuhusu watu wakihusika katika tabia hizo, ningejikumbusha kwamba sipaswi kuasi dhidi ya Mungu kama walivyofanya. Aidha, nilikuwa mwangalifu katika jitihada zangu zote na nilishikilia kazi zote nilizopewa na kanisa. Sikurudi nyuma kutoka kwa wajibu wangu wakati niliposhughulikiwa na kupogolewa wala kuondoka kutoka kanisani nilipojaribiwa, bila kujali shida. Kwa hiyo, niliamini kwamba sikuwahi kuasi dhidi ya Mungu kamwe. Nilihisi kuwa nilikuwa nimepata hadhi fulani tayari na nilikuwa na hakika kwamba ningemfuata Mungu mpaka mwisho na hatimaye kufanikisha wokovu.

Siku moja wakati wa ukuzaji wa roho, nilisoma hili katika mahubiri: “Kuna aina mbalimbali za uasi dhidi ya Mungu. Aina moja ya uasi ni kuenda kinyume na mapenzi Yake au kwenda kinyume na maneno Yake; aina nyingine ni kuwa na tabia ya kiburi, kukosa Mungu katika moyo wa mtu, na hivyo kujivunia na kuwa na uhasama na Mungu—huu ni uasi wa kutomtii na kutomjali; kuna aina moja zaidi, ambayo ni uasi wa kumsaliti na kumtelekeza Mungu. … Tabia za uasi ambazo sisi huziongelea mara kwa mara katika ushirika hurejelea hasa aina mbili za kwanza. Hii ni kwa sababu wale ambao humsaliti na kumtelekeza Mungu hawako ndani ya mawanda ya wokovu wa Mungu, na tabia za uasi zilizotajwa katika maneno ya Mungu pia ni za aina mbili za kwanza; aina ya tatu ya uasi haijatajwa. Hatupaswi kuelewa visivyo au kutafsiri vibaya dhamira za Mungu, tukiamini kuwa ni kumsaliti tu au kumtelekeza tu kunakoweza kuitwa kuasi dhidi ya Mungu, kana kwamba kwenda kinyume na neno Lake au kuwa na tabia ya kiburi si aina ya uasi. Huu ni ufahamu wa upande mmoja kabisa! Hivyo uasi hasa ni nini? Watu wanapaswa kuutambuaje? Kwa mujibu neno la Mungu, vitu vyote ambavyo havilingani na Mungu ni maadui Wake, na vitu vyote vinavyoenda kinyume na maneno ya Mungu vinaasi dhidi ya maneno Yake. Kuasi dhidi ya maneno ya Mungu ni kuasi dhidi ya Mungu, na kutenda kama adui Yake pia ni kuasi dhidi Yake. Yaelekea kuwa kanuni hizi mbili hazilingani na dhana za kibinadamu, lakini hiki hasa ni kiini cha tatizo” (Ushirika Kutoka kwa wa Juu). Baada ya kusoma ushirika, nilitambua kuwa kuasi dhidi ya Mungu haikuwa kumsaliti Yeye tu, kutelekeza kanisa, au kuziacha kazi za mtu. Badala yake, kukiuka mapenzi ya Mungu au neno Lake, na kumpinga Yeye pia ni aina za uasi. Chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, nilianza kutafakari juu ya matendo yangu. Mungu hutaka tufuatilie ukweli na kubadilika katika tabia tunapotimiza wajibu wetu. Hata hivyo, nimelenga kazi na kupata hadhi ya juu ndani ya kanisa ninapotimiza wajibu wangu. Mungu hutusihi tufanye kazi zetu kwa uaminifu, tufuate mapenzi Yake wakati tunapokabiliwa na shida, na tuunyime mwili ili kuutenda ukweli. Hata hivyo, mimi daima hutafuta njia ambayo inahitaji jitihada kidogo kuliko zote katika kutimiza wajibu wangu, nikimdanganya Mungu na utepetevu wangu. Mimi huujali tu mwili wangu wakati wa shida, kulalamika juu ya matatizo na kuzembea katika wajibu wangu. Hata nimefikiria kukata tamaa kabisa kama njia ya kuutoroka wajibu wangu. Mungu huhitaji uaminifu kamili na kujitolea kamili. Mbele ya Mungu, mawazo yangu mara nyingi hushughulika na familia yangu na jamaa zangu. Mungu hutusihi tujifunze mafundisho katika vitu vyote na kuingia katika ukweli wa neno Lake ili tuweze kukamilishwa na Mungu. Wakati ninapokabiliwa na watu au mambo yasiyofaa, mimi husita kwa fikira kwamba vitu vyote ni sehemu ya mpango wa Mungu na hujipata daima nikiyumba kati ya mema na mabaya. Mungu hututaka tuingie katika ukweli na kukubali wokovu wa Mungu katika hali mbalimbali na majaribu ya shida ambayo Yeye ametupangia. Ninapokabiliwa na kushughulikiwa, kupogolewa, kipingamizi, au kushindwa, mimi huelewa visivyo na kumlaumu Mungu. Mimi huhisi kukata tamaa kuelekea barabara iliyo mbele, kupoteza imani kwa Mungu, na hata hufikiria kuacha kanisa. Mungu hutusihi tuwe makini, watu wa vitendo na wa kufaa katika maisha yetu ya kiroho. Mimi, hata hivyo, mara nyingi hutumia kanuni na taratibu, na kutenda kaida za dini. Mungu hutusihi tumtukuze na kumshuhudia Yeye katika kazi yetu na kuwaleta watu mbele Yake. Hata hivyo, mimi hujitukuza na kujishuhudia mwenyewe, nikiwaleta wengine mbele yangu ili wanipende na kunistahi. Mungu hutusihi tutumie ukweli ili kutatua matatizo yetu. Mimi huwa ninajigamba na kuzungumza juu ya elimu na mafundisho ya dini, kuwawekea wengine mipaka kwa kutumia kanuni, kutatua matatizo kulingana na njia za mwanadamu, na kuwakandamiza wengine kwa kutumia hadhi. Mungu hutusihi tufanye kazi zetu kwa mujibu wa mipango ya kazi. Kwa kawaida mimi hufanya kazi yangu kwa msingi wa nia zangu, kufanya vitu kwa njia ambayo ninaona kuwa inafaa. … Si vitendo hivi vyote vinakiuka mapenzi ya Mungu na neno Lake na viko katika upinzani kwa Mungu? Si vitendo hivi hufanyiza uasi dhidi ya Mungu?

Kwa wakati huu, siwezi kujizuia kujisikia mwenye hisia ya woga. Yaelekea kuwa niliasi dhidi ya Mungu bila kufahamu katika vitendo vyangu vyote huku nikiamini kwa kukosea kuwa uasi ulikuwa na maana ya kulisaliti kanisa, kulitelekeza kanisa, au kuziacha kazi za mtu. Kwa kujipujua nilifikiri kwamba kimo changu kiliniruhusu kuasi dhidi ya Mungu. Nimekuwa mgeni kwangu mwenyewe, na ufahamu wangu wa neno la Mungu ni wa urahisi na wa juu juu. Maneno ya Mungu yanasema, “Mungu ameifunua asili na kiini cha mwanadamu, lakini mwanadamu anafahamu kwamba njia yake ya kuyatenda mambo na njia yao ya kusema ni yenye mawaa na yenye kasoro; kwa hiyo ni kazi yenye kutumia juhudi nyingi kwa watu kutia ukweli katika vitendo. Watu wanafikiria kwamba makosa yao ni udhihirisho wa muda tu, ambao unafunuliwa bila kujali, badala ya kuwa ufunuo wa asili yao” (“Kuifahamu Asili na Kuutia Ukweli Katika Vitendo” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). “Asili ya mtu ni maisha yake, ni kanuni ambayo anaitegemea ili kuendelea kuishi, na anashindwa kuibadilisha. Jinsi ilivyo hali ya usaliti—kama unaweza kufanya kitu ili kumsaliti ndugu au rafiki, hii inathibitisha kwamba ni sehemu ya maisha yako na hali ambayo ulizaliwa nayo. Hiki ni kitu ambacho hakuna mtu anaweza kukikana” (“Tatizo Kubwa Sana: Usaliti (1)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Hilo ni kweli pasipo mashaka. Si mimi kabisa ni aina ya mtu wa kuhangaika juu ya mambo madogo bila kuelewa kwa dhahiri asili yangu? Tabia za watu hutawalwa na asili yao, na tabia yao ni dhihirisho la asili yao. Ikiwa uasi umeandikwa katika lugha ya mficho ndani ya asili ya mwanadamu, basi mtu ataasi dhidi ya Mungu bila kuepuka. Hili si suala la kuwa na tahadhari. Lakini, sijajishughulisha na kuitambua asili yangu. Badala yake, nimeridhishwa na kushikilia matendo fulani ya nje, ambayo hunizuia kutafuta ukweli na kubadilisha tabia yangu, ingawa nimemfuata Mungu kwa miaka mingi. Kwa kawaida nimeishi na asili ya uasi. Nikiendelea kufanya hivyo, kwa kuzingatia mazingira mazuri, bila kuepuka nitatawaliwa na asili yangu, kulisaliti na kuliacha kanisa. Hii ni njia hatari kweli!

Ee Mungu, asante kwa kunionyeshea ukweli kuhusu imani zangu zenye makosa kuhusu uasi dhidi Yako. Uliniruhusu nielewe kwamba kutelekeza na kukiuka neno Lako ni aina za uasi, na ukanionyesha kuwa mimi niko katika hatari ya kuasi dhidi Yako, kukusaliti, na kukutelekeza. Kutoka leo kwendelea, niko tayari kuzingatia neno Lako na kulenga juhudi zangu kwa kutafakari juu ya maana halisi ya neno Lako, ili kwa kweli kuelewa kiini cha ukweli na kujiruhusu kuingia na kutenda ukweli kwa usahihi. Nitajitahidi kutetea neno Lako katika hali zote na kurekebisha ukaidi wangu.

 

Chanzo:  Kanisa la Mwenyezi Mungu

 

 

Views: 136 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: Kanisa, Ushuhuda wa Maisha, ukweli | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar