9:08 AM
46. Kupitia Upendo Maalum wa Mungu

Jiayi Mji wa Fuyang, Mkoa wa Anhui

Asili yangu ni ya kiburi hasa; bila kujali ninafanya nini, mimi daima hutumia werevu na ujuzi wa kubuni ili kuonyesha akili yangu na kwa hiyo mara kwa mara hukiuka mipango ya kazi ili nifanye mambo kwa njia yangu mwenyewe. Mimi ni mwenye kiburi hasa kuhusu kuchagua watu kwa cheo fulani. Ninaamini kuwa nina talanta ya kipekee na umaizi ambavyo hunisaidia daima kumchagua mtu sahihi. Kwa sababu ya hili, nilipomchagua mtu, singechunguza kwa dhati ili kuelewa hali zote za mtu niliyetaka kumchagua. Pia singewapima kwa makini watu ambao ninataka kuchagua kulingana na maadili yanayohusiana. Matokeo ya hili yalikuwa ni kwamba niliishia kuwachagua watu fulani wenye hila na udanganyifu waliozungumzia tu masomo na mafundisho ili kujichukulia majukumu muhimu katika kanisa. Hili lilisababisha hasara kubwa kwa kazi na pia kwa maisha ya ndugu zangu wa kiume na wa kike. Hatimaye, kutokana na ukosefu wangu wa kazi halisi katika huduma ya Mungu, nilikataliwa na Mungu. Nilipoteza kazi ya Roho Mtakatifu na kuondolewa kwa huduma.

Nilipopata habari kwamba ningepaswa kubadilishwa, niliduwaa. Ilikuwa vigumu kufikiria kwamba jambo kama hili lingenitokea. Baadaye, nilianza kutomwelewa Mungu na kumhoji: Kanisa lilinibadilisha na halikunipa kazi yoyote. Ilionekana kama shida yangu ilikuwa mbaya sana. Iliwezekana kwamba ningefukuzwa. Watu wengine walikuwa wamefukuzwa hapo zamani kwa sababu walikuwa wamefanya kazi bila uangalifu na walimdanganya Mungu na walidakiza pakubwa na kusumbua kazi ya kanisa. Na wengine walikuwa wapinga Kristo kwa sababu walijitukuza, wakajishuhudia, na wakashindana na Mungu kwa ajili ya watu Wake waliochaguliwa. Hata zaidi si ningefukuzwa leo kwa sababu nimefanya kazi kwa kuzembea, nikamdanganya Mungu, nikajiinua, nikajishuhudia, na nikadakiza pakubwa na kusumbua kazi ya kanisa? Kwa kuona baa hili nililolisababisha, nilitetemeka kwa hofu. Moyo wangu ukasema mfululizo: Nimekwisha. Wakati huu nimekwisha kabisa. Nilikuwa nimempinga na kumkosea Mungu mara nyingi. Mungu bila shaka hangeninusuru. Ingawa Mungu alikuwa amesema kuwa Yeye anafanya kila kitu anachoweza kuwaokoa wanadamu, ilihusika na wale ambao walikuwa wamepotoka kidogo na wale waliofanya makosa madogo. Mtu mwenye kiburi na mwenye majivuno kama mimi mwenyewe ambaye hakuweza kumtambua Mungu na kutenda aina zote za dhambi bila shaka angepatwa na adhabu ya Mungu. Hata kama ningejitahidi kufanya mwanzo mpya, Mungu hangenisamehe, kwa sababu matendo yangu yalikuwa yamesababisha Mungu kupoteza tumaini nami na kumhuzunisha Yeye mno sana…. Pasipo kujua, nilizama katika maumivu na kukata tamaa.

Katika maumivu yangu makubwa, nilitamani kuwa kanisa lingenipa fursa nyingine ya kutimiza wajibu fulani. Lakini kila wakati wazo hili lilipokuja katika mawazo yangu, maneno “dhambi nzito” yangetangua na kugubika dalili yoyote ya matumaini. Maumivu, kujilaumu, mapambano, na matamanio yangu yalinitesa, yakanisababishia maumivu mengi kiasi kwamba sikutaka kuishi. Nilikaribia kuchanganyikiwa katika kukata tamaa kwangu. Wakati huu tu, nilisoma neno la Mungu likisema, “Mungu hapendi waoga; Anapenda watu wenye azimio. Hata kama umeonyesha upotovu mkubwa, hata kama umepitia barabara nyingi zilizopinda, au hata ikiwa njiani umekuwa na makosa mengi au umemkataa Mungu—au kuna watu wengine ambao wanamkufuru Mungu mioyoni mwao au wanamlaumu Yeye, wana mgogoro naye—Mungu hatazami jambo hili. Mungu huangalia tu ikiwa siku moja mtu ataweza kubadilika au la. … Ni kwamba mapenzi ya Mungu ya kuwaokoa wanadamu ni ya kweli. Anawapa watu fursa za kutubu na fursa za kubadili, na wakati wa mchakato huu, Anawaelewa watu na Anajua udhaifu wao kwa kina na kiwango cha upotovu wao. Anajua kwamba watajikwaa. … Anaelewa matatizo ya kila mtu, udhaifu, pamoja na mahitaji yake. Hata zaidi, Anaelewa shida gani kila mtu atakabiliwa nazo katika mchakato wa kuingia katika mabadiliko, na aina zipi za udhaifu na kushindwa zitakazotokea. Hili ni jambo ambalo Mungu anaelewa zaidi. Ndiyo maana inasemwa Mungu huona ndani ya vina vya mioyo ya watu. Haijalishi wewe ni dhaifu kiasi gani, mradi huliachi jina la Mungu, mradi humwachi Mungu au njia hii, daima utakuwa na fursa ya kufikia mabadiliko katika tabia. Na ikiwa tuna fursa ya kufikia mabadiliko katika tabia basi tuna matumaini ya kuendelea kwetu kuishi. Ikiwa tuna matumaini ya kuendelea kwetu kuishi, tuna matumaini ya kuokolewa na Mungu” (“Ni Nini Maana ya Mabadiliko Katika Tabia na Njia Kuelekea Mabadiliko Katika Tabia” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Nilisikiliza pia maneno haya kutoka kwa mahubiri, “Mungu anafanya yote Anayoweza ili kuwaokoa wanadamu. Hasa wakosaji, watu hudhani kuwa wamepita kiwango cha kuokolewa, lakini Mungu hayuko tayari kukata tamaa juu yao na bado anataka kuwaokoa. Watu wengine wana makosa makubwa. Mungu aliwaambia, 'Unahitaji tu kurudi kwa kujitolea ulikokuwa nako kabla na kufuatilia ukweli. Bado Nataka kukuokoa.' Bila kujali ni makosa gani uliyo nayo, mradi una dhamira ya kutomwacha Mungu kamwe na hamu ya kutafuta wokovu, basi Mungu hatakata tamaa na wewe” (“Jinsi ya Kujua Kristo Ndiye Ukweli, Njia, na Uzima” katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha II). Maneno haya yalionekana kuwa umande mzuri ambao ulirowesha ukame wa kudumu katika moyo wangu. Niliangua kilio na kumamia. Sikutambua ni mara ngapi “haiwezekani” liligeuka bila kutarajia kuwa bora. Mungu alisema kwamba bado Anataka kuniokoa nisipoacha ukimbizaji wangu, nitafute kutubu, na nisiondoke au kumtelekeza Yeye bila kujali hali yangu. Sikuweza kujizuia kusujudu mbele ya Mungu: “Ee Mungu! Ninakuamini na kukufuata, na bado ninakupinga na kukuasi kila mara. Mara kwa mara mimi hutenda kulingana na mapenzi yangu ninapotekeleza wajibu wangu, na mimi hudakiza na kuvuruga kazi ya kanisa; lakini umenivumilia na kunisamehe. Umenipa fursa nyingine ya kutubu na kuokolewa. Ee Mungu! Upendo Wako umeondoa kutoelewa kwangu na maswali yangu Kwako. Umesababisha moyo wangu unaokufa kupona na kuinuka kwa kutoka kwa uhasi wa kuzidi kiasi, maumivu na kukata tamaa. Umeitia moto tena tamaa yangu ya uzima mara nyingine —kutafuta wokovu. Ee Mungu! Upendo Wako kwangu ni wa kina sana, ni mkubwa sana! Kwa sababu ya upendo Wako kwangu, umesamehe makosa yangu yote, umesamehe ukinzani wangu wote na upinzani. Umefanya kazi Yako ya wokovu kwangu kupitia uvumilivu Wako mkubwa. Ee Mungu! Wewe ni mkubwa sana, ni mzuri sana! Siwezi kunena ninapokabiliwa na Upendo wako, naona haya na siwezi kuonyesha uso wangu. Ninajisikia kwa undani kwamba ningeona haya kuishi katika uwepo Wako. Kwa wakati huu, naweza tu kukutumia shukrani na sifa zangu za dhati. Ninaweza tu kukupa Wewe wimbo wa moyo wangu: “Upendo wako umenifanya nisiweze kuchagua kitu kingine chochote, sitakuacha Uwe na wasiwasi tena kunihusu. Watu wapotovu hufurahia upendo Wako mno. Wewe ndiwe upendo pekee moyoni mwangu, pekee ninayempenda, ninayemheshimu sana, na kumtegemea. Bila upendo Wako, nina maumivu tu na siwezi kuendelea kuishi. Ni furaha iliyoje kukujua Wewe maisha yangu yote. Bila kujali hali zangu zikoje, nitazifuata nyayo Zako na kufuatana Nawe ili kukufariji. Nikiwa katika maumivu makali, mimi pia nataka kuwa shahidi na kukuridhisha Wewe. Kuteseka na usafishwaji husababisha moyo wangu kuwa karibu na Wewe. Nina furaha milele kuwa na Wewe moyoni mwangu.”

Baada ya kuondosha mawazo yangu mabaya kuhusu Mungu, nilianza kutulia na kuchunguza tabia yangu ya zamani: Katika kazi yangu, sikuwahi kamwe kumtegemea Mungu wala kumheshimu. Sikutafuta mapenzi ya Mungu na sikufanya kulingana na mipango ya kazi au mahitaji ya kanisa. Nilitegemea kabisa akili yangu mwenyewe, sifa za ndani, na ujuzi wa kufanya mambo kwa njia yangu mwenyewe. Sikuwahi kamwe kuona au kushughulikia mambo kulingana na neno la Mungu, na sikutafuta kanuni za kazi yangu. Nilitegemea hisia zangu na mawazo yangu ili kuamua na kukisia. Sikuwahi kamwe kushauriana na wengine na mara nyingi nilifanya mambo yangu mwenyewe. Hata kama nilishauriana na wengine, ilikuwa tu ili kwamba ningeonekana kuwa mnyenyekevu. Kwa uhalisi, tayari nilikuwa na mpango katika mawazo yangu na kwa sababu ya hili, mara chache niliyashirikisha mawazo ya watu wengine. Singeweza kutekeleza mipango ya kazi kutoka walio juu vizuri kama hawangefuata mawazo yangu na kama mtu angejaribu kunishughulikia na kunipogoa, hata zaidi sikuwa tayari kulikubali. Mimi hasa nilitaka kuwa bora zaidi; bila kujali nilichokifanya nilitaka kuwapita wengine. Niliamini kwamba nilikuwa bora zaidi kuliko kila mtu na kwamba hakuna kazi katika kanisa ambayo sikuweza kufanya na kwamba kila kitu nilichokifanya kilikuwa kizuri. … Kwa sababu ya kudhibitiwa na asili yangu ya kiburi, nilitegemea asili ya Shetani ambayo ilikuwa ndani yangu kucharuka katika kazi yangu kwa miaka mingi. Kimsingi sikutafuta ukweli na sikusisitiza kujijua. Nilitafuta nafasi nzuri kikamilifu, na nilitaka kuwa kiongozi mkuu. Kwa ajili ya hilo, sikuelewa kikamilifu tabia ya Mungu wala kiini cha Mungu. Sikuwa hata na kiwango kidogo cha heshima au uchaji kwa Mungu. Nilitenda kwa uzembe mbele ya Mungu na hakuna kilichonizuia. Ningethubutu kusema chochote na kufanya chochote. Sikutambua kwamba nilikuwa nikichukua nafasi ya mchungaji wa uongo; nilikuwa nachukua njia ya kumtumikia Mungu huku nikimpinga. Ingawa ndugu wa kiume na wa kike walinikumbusha mara nyingi, sikukubali msaada wao uliokuwa na nia nzuri. Nilikuwa na kiburi mno na niliendelea katika njia zangu. Kwa sababu ya nyakati nyingi nilipompinga Mungu na nikaenda kinyume na Yeye, niliichochea hasira ya Mungu na hatimaye niliondolewa kwa huduma, ambayo ilinielekeza kujiwazia.

Baada ya kuchunguza jambo hili, hatua kwa hatua nilianza kuamka kutoka kwa mzubao wangu. Wakati huu wote, Mungu alikuwa ameweka mawazo mengi katika mambo yote yaliyonipata kwa nia ya kunikomboa. Sikuweza kujizuia kusujudu tena mbele ya Mungu: Ee Mwenyezi Mungu, nakushukuru Wewe! Ingawa kubadilishwa wakati huu kulihisi tu kama kufa na maumivu yangu yalikuwa yasiyolinganishika, kulitumika kama kisingizio cha mimi kupata uzoefu wa upendo Wako mkubwa na wokovu kwangu. Kama singekuwa nimebadilishwa wakati huu, ningekuwa bado ninaishi ndani ya dhana na mawazo yangu mwenyewe, nikiendelea kufanya mambo kwa njia isiyo sahihi. Bado ningeamini kwamba kutelekeza familia yangu na kazi ili kufanya kazi katika kanisa kulikuwa kukuhudumia kwa uaminifu. Singekuwa nimetafakari juu ya mwenendo wangu, na singetambua kwamba huduma yangu ilikuwa kukupinga Wewe. Kama mambo yangeendelea jinsi hii, ningekuwa tu mwenye kiburi na mwenye majivuno. Hatimaye ningekuwa nikikupinga kama mpinga Kristo na ningepaswa kukabiliwa na adhabu yako. Ee Mungu, upendo Wako kwangu ni mkubwa sana na halisi! Ubadili wa leo ni jinsi Unavyotaka kuniokoa kwa hakika. Upendo wako wa kuadibu umeushinda moyo wangu. Ninakushukuru Wewe kutoka moyoni mwangu kwa kuniokoa na kunilinda. Ninakushukuru Wewe hata zaidi kwa kunisababisha kwa hakika kupata uzoefu kupitia kwa ufunuo Wako kwamba tabia Yako ya haki haiwezi kuvumilia kosa; ninakushukuru kwa kuniruhusu nione mapenzi makubwa ya baba Uliyo nayo katika vipigo vikatili na majaribu machungu ya mwanadamu. Wakati huo huo, umeniruhusu pia kutambua kiini changu kipotovu na kuona kwamba nimepotoshwa sana na Shetani. Asili ya kiburi imekita mizizi kwa kina ndani yangu na ninahitaji sana kuadibu Kwako, hukumu, majaribu, usafishwaji, na hata adhabu Yako na laana ili kunisafisha na kuniokoa. Ni kwa njia ya kazi hii tu ambapo ninaweza kuibuka na heshima kuu Kwako na kulindwa na kutakaswa. Ee Mungu, tangu siku hii kwendelea, niko tayari kutafuta ukweli kwa bidii na kwa kweli kuitii kazi Yako. Nitakubali hukumu Yako na kuadibiwa. Bila kujali jinsi gani Wewe hunitendea, nitajiweka chini Yako kikamilifu na kuikubali mipango Yako. Sitaelewa visivyo wala kulalamika. Nitakuwa mtu halisi na kuishi na thamani na kusudi.

Chanzo:  Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kupitia Upendo Maalum wa Mungu

Views: 121 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: mapenzi ya Mungu, ukweli, hukumu kwa Mungu | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar