3:40 AM
1. Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake

1. Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake

Hu Ke Mji wa Dezhou, Mkoa wa Shandong

Wakati wowote nilipoona maneno haya yaliyosemwa na Mungu,nilihisi kuwa na wasiwasi:“ Kila sentensi Niliyoizungumza ina tabia ya Mungu ndani yake。Mngefanya vizuri endapo mngetafakari kuhusu maneno Yangu kwa umakini,na kwa kweli mtafaidi pakubwa kutoka kwa maneno hayo “(”Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu“katika Neno Laonekana katika Mwili)。Nilihisi kuwa na wasiwasi kwa sababu kuelewa tabia ya Mungu ni muhimu sana yote kwa ufahamu wa mwanadamu wa Mungu na kutafuta kumpenda na kumridhisha Yeye。Lakini wakati wa kula na kunywa maneno ya Mungu,siku zote nilihisi kama tabia ya Mungu ilikuwa dhahania mno,na sikujua jinsi ya kuielewa。Baadaye,kupitia kwa ushirika kutoka kwa kiongozi wangu,nilikuja kujua kwamba ni lazima nielewe kile ambacho Mungu anapenda na kile Anachokichukia kutoka kwa maneno Yake,na hivyo kuelewa tabia ya Mungu。Baadaye nilijaribu kwa muda kuweka jambo hili katika matendo na niliona matokeo。Lakini bado nilihisi kuchanganyikiwa kuhusu maneno ya Mungu,“ Kila sentensi Niliyoizungumza ina tabia ya Mungu ndani yake。“na sikuwa na wazo la jinsi ya kuyaelewa hasa。

Siku moja, nilisoma maneno haya katika mahubiri: “Tabia ya Mungu ina vipengele vingi. Ina kile Mungu anacho na alicho, fikra Zake, mawazo Yake, kufikiria Kwake na hekima. Ina njia ya Mungu kwa kila aina za watu, kama vile hisia Zake za huruma na utunzaji, na bado zaidi hasira Yake kwelekea kwa uasi wa wanadamu na upinzani. Kwa sababu kila sentensi ya Mungu ina kufikiria Kwake, hekima Yake na mawazo Yake, kwa sababu zote zina usuli na chanzo cha maneno Yake, kwa sababu zote huonyesha mwenendo wa Mungu kuwaelekea wanadamu, kukiwa hakuna hata sentensi moja ambayo haina msingi, ni kitu cha asili sana kwa kila sentensi kuwa na tabia ya Mungu. Kila neno wanadamu husema huonyesha tabia yao ya maisha, kwa hivyo kila neno la Mungu halitakuwa na tabia Yake hata zaidi? Hili ni rahisi kuelewa, lakini jinsi ya kuligundua na kulijua si rahisi kama watu wanavyofikiri. Kama, wakati wa kusoma maneno ya Mungu, mtu hajaribu kuyaelewa vya kutosha, haweki jitihada za kutosha au hana uzoefu wa kutosha, basi tabia ya Mungu haitakuwa rahisi kutambua, sembuse kuelewa. Kinachohitajika basi ni kwa wanadamu kujituliza mbele ya Mungu na kuweka mioyo yao katika maneno ya Mungu kabisa, na kusoma kwao na kujaribu kuyaelewa maneno ya Mungu kufanywe wakati wa maombi; kisha utakuja polepole kugundua hali ya akili katika maneno ya Mungu. Huu ni mwanzo wa kuingia” (Ushirika Kutoka kwa wa Juu). Niliposoma ushirika huu, kila kitu kilieleweka. Niligundua kwamba tabia ya Mungu ina mambo mengi: Ina kile Mungu anacho na alicho, fikra Zake na mawazo Yake, kufikiria Kwake na hekima Yake, pamoja na mwenendo Wake kwa watu wa aina yote, na kadhalika. Aidha, kila sentensi ya Mungu ina usuli na chanzo cha kila neno Lake, bila ya sentensi moja kutokuwa na msingi, na kila kitu ambacho Mungu hufanya na kila sentensi Anayoizungumza ni maonyesho ya kawaida ya yote Aliyo katika maisha. Ufahamu wangu wa tabia ya Mungu, kwa upande mwingine, ulikuwa umezuiwa tu kwa kile ambacho Mungu anapenda na kile Anachochukia. Aina hii ya ufahamu ilikuwa ya upande mmoja mno kwa hiyo haikuweza kufikia ufahamu wa tabia ya Mungu kutoka kwa kila sentensi Yake. Mbali na hili, nilielewa pia kwamba, kama nilitaka kuelewa tabia ya Mungu kutoka kwa kila sentensi Yake, nilihitaji kujituliza mbele ya Mungu na kufanya jitihada nyingi zaidi kujaribu kuyaelewa maneno ya Mungu. Aidha, nilihitaji kuomba na kutafuta mwongozo mbele ya Mungu, nikizingatia kuelewa hali ya akili katika maneno ambayo Mungu ameyazungumza na vilevile usuli na chanzo cha matendo ya Mungu.

Nakushukuru kupata nuru ya Mungu na mwangaza ambao uliniruhusu kutambua mambo haya, na kisha baadaye nilianza kuzingatia kutenda na kuingia katika kipengele hiki. Siku moja, nilisoma kifungu cha maneno ya Mungu: “Haijalishi kazi hii ni muhimu au si muhimu lakini imejikita katika mahitaji ya mwanadamu, na uhalisi wa upotovu wa mwanadamu, na uzito wa kutotii kwa Shetani na usumbufu wake katika kazi. Mhusika sahihi anayeifanya kazi ametabiriwa na asili ya kazi yake, na umuhimu wa kazi. Unapokuja umuhimu wa kazi hii, kwa misingi ya mbinu ya kutumia—kazi inayofanywa moja kwa moja na Roho, au kazi inayofanywa na Mungu mwenye mwili, au kazi inayofanywa kupitia mwanadamu—ya kwanza kuondolewa ni kazi inayofanywa kupitia mwanadamu, na kulingana na asili ya kazi, na asili ya kazi ya Roho dhidi ya ile ya mwili, hatimaye inaamuliwa kwamba kazi inayofanywa na mwili ni ya manufaa zaidi kwa mwanadamu kuliko kazi inayofanywa moja kwa moja na Roho, na inakuwa na manufaa zaidi. Hili ni wazo la Mungu wakati wa kuamua ama kazi ifanywe na Roho au ifanywe na mwili” (“Mwanadamu Aliyepotoka Anahitaji Zaidi Wokovu wa Mungu Mwenye Mwili” katika Neno Laonekana katika Mwili). Nilipojaribu kukielewa kifungu hiki, nilihisi kana kwamba nilikuwa nimegundua ukarimu mkubwa. Maneno ya Mungu huonyesha maendeleo ya kufikiria Mungu wakati huo, kufikiria utaratibu gani wa kutumia kwa kazi katika siku za mwisho. Wakati wa kufikiria Kwake, jambo la kwanza Mungu alifikiria ni njia gani ya kutumia ambayo ingekuwa ya manufaa zaidi kwa mwanadamu katika kazi hii, jinsi gani ya kufikia matokeo ya wokovu wa mwanadamu na ni nini cha kumfanya Shetani akubali kushindwa, kwa hivyo akimshinda Shetani na kuwaleta watu ambao wamedhuriwa kwa kina sana katika wokovu kamili. Wakati wa mchakato huu mzima wa fikra, Mungu daima alimfikiria mwanadamu na kamwe hakuyafikiria maslahi Yake mwenyewe au usalama. Mungu alijua waziwazi kupata mwili Kwake kungepatwa na shida nyingi, lakini hili halikuwa la kufikiriwa ilipofikia kuwaokoa wanadamu. Badala yake, bado Alichagua, kwa msingi wa mahitaji ya wanadamu na uhalisi wa upotovu wa wanadamu, utaratibu wa Mungu kupata mwili wa kutekeleza kazi ya siku za mwisho. Yeye huhatarisha janga kubwa kuingia katika pango la chui milia, Yeye huyapitia mateso makali na ukimbizwaji na joka kubwa jekundu, huvumilia dhuluma na kukufuru kwa dini na madhehebu mbalimbali, na pia huvumilia upinzani, uasi na kutokuelewana kwa wale wetu ambao hufuata. Majeraha na mashambulizi yaliyouumiza moyo wa Mungu na fedheha ambayo Mungu huvumilia kwa kweli ni mambo ambayo hakuna mtu anayeweza kuyaelewa. Kila kitu ambacho Mungu huonyesha na kufichua ni chote Alicho katika maisha: kujitolea Kwake kwa wanadamu kwa kujinyima na kulipa Kwake gharama kwa ajili yao. Ukuu wa Mungu na kujinyima vimefichuliwa kwa kawaida katika kazi Yake na kila sentensi Yake, na hivi pia hujumuisha rehema kubwa ya Mungu na upendo usio na ubinafsi. Upendo wa Mungu kwa wanadamu sio tu maneno matupu, lakini ni gharama ya utendaji ambayo Yeye hulipa. Wakati huo, nilikuwa na ufahamu dhahiri kwamba Mungu kwa kweli ni mkubwa sana na wa kupendeka sana! Kwa hiyo, ingawa nilikuwa nimesoma maneno haya ya Mungu hapo awali, sikuwahi kuelewa usuli wa maneno ambayo Kristo aliyanena au yote yaliyofichua, wala sikuwa nimeuelewa upendo wa Kristo kwa wanadamu. Ni sasa tu nilipokuwa na ufahamu kiasi wa kweli wa maneno haya ya Mungu: “Kila sentensi Niliyoizungumza ina tabia ya Mungu ndani yake.

Kabla,kwa kuwa sikuwa nimewahi asilani kuutuliza moyo wangu au kujitahidi kuyaelewa maneno ya Mungu,nilipoteza fursa nyingi nzuri sana za kumjua Mungu,nyingi sana kiasi kwamba hata leo bado nina dhana nyingi na suitafahamu kumwelekea Mungu,na bado nimetenganishwa na Yeye。Ni sasa tu ninapoelewa kwamba kama napenda kuielewa tabia ya Mungu,ni lazima nijaribu kwa bidii kuelewa na kutafuta ukweli ndani ya kila sentensi ya Mungu。Kwa njia hii,hakika nitafaidika sana。Kuanzia leo kwendelea,natamani kuzingatia kuweka juhudi nyingi zaidi katika maneno ya Mungu,na kutafuta hivi karibuni kuwa mtu ambaye ana ufahamu kiasi wa Mungu。

Chanzo:Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake

Views: 116 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: tabia ya Mungu, Maneno ya Mungu | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar