7:29 PM
Swahili Christian Video "Mtoto, Rudi Nyumbani" | Hakuna Wokovu Ila Kupitia Kwa Bwana

Swahili Christian Video "Mtoto, Rudi Nyumbani" | Hakuna Wokovu Ila Kupitia Kwa Bwana

Li Xinguang ni mwanafunzi wa shule ya upili ya ngazi ya juu. Alikuwa mvulana mwenye busara na mwenye tabia nzuri tangu alipokuwa mdogo. Wazazi wake na walimu wake walimpenda sana. Alipokuwa akienda katika shule ya kati, alipumbazwa na michezo ya kompyuta ya mtandaoni. Angekosa kwenda darasani mara kwa mara ili aende kwenye chumba cha mtandao. Wazazi wake walifanya kila juhudi kumsaidia kuyaondoa mazoea yake ya michezo. Kwa bahati mbaya, uzoefu wa Li Xinguang ulizidi kuwa mbaya zaidi na zaidi. Alikuwa mwenye kuvunjika moyo na polepole akabadilika na mvulana msumbufu. … Wazazi wa Li Xinguang walipohisi kuwa hawakujua la kufanya, walisikia kwamba Mungu ana uwezo wa kuwaokoa watu, Akiwasaidia kuwaondolea mazoea ya michezo na kujinasua kutokana na upotoshaji wa Shetani. Kama matokeo, waliamua kumwamini Mungu na wakangoja kwa hamu Mungu amwokoe mwana wao. Kutoka kwa maneno ya Mungu, walielewa chanzo cha upotovu na mkengeuko wa mwanadamu. Waliona ukweli wa giza la mwanadamu na uovu na wakaelewa kwamba ni Mungu tu Anayeweza kuwaokoa watu na kuwaweka huru kutokana na upotoshaji wa Shetani na mateso. Kila alichohitaji kufanya Xinguang kilikuwa ni kumwamini Mungu na kuuelewa ukweli, na angeweza kuvunja mazoea yake ya michezo. Kama matokeo yake, walieneza injili kwa Xinguang na kumwongoza Xinguang kusoma maneno ya Mungu. Walimwomba Mungu na kumsihi amwokoe mwana wao na kumsaidia avunje mazoea yake ya michezo. … Baada ya pambano, Xinguang alianza kumwomba Mungu na kumtegemea Mungu. Chini ya uongozi wa maneno ya Mungu, hatimaye aliondokana na mazoea yake ya michezo na kujinasua toka kwa upotovu wa Shetani na mateso. Huyu mwana aliyekuwa amepotoea bila matumaini katika michezo ya mtandaoni na vyumba vya mtandao mwishowe alikuja nyumbani!

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana. 

Views: 94 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: Mfululizo wa Filamu za Injili | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar