4:45 AM
Neno la Mungu | “Yule tu Anayepitia Kazi ya Mungu Ndiye Anayemwamini Mungu Kweli” (Dondoo)

Neno la Mungu | “Yule tu Anayepitia Kazi ya Mungu Ndiye Anayemwamini Mungu Kweli” (Dondoo)

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuchunguza kitu cha aina hii sio vigumu, lakini kunahitaji kila mmoja wetu ajue ukweli huu: Yeye Aliye mwili wa Mungu Atakuwa na dutu ya Mungu, na Yule Aliye Mungu katika mwili Atakuwa na maonyesho ya Mungu. Kwa maana Mungu Hupata mwili, Ataleta mbele kazi Anayopaswa kufanya, na kwa maana Mungu Amepata mwili, Ataonyesha kile Alicho na Ataweza kuuleta ukweli kwa mwanadamu, kumpa mwanadamu uhai, na Amwonyeshe mwanadamu njia. Mwili usio na dutu ya Mungu kwa kweli sio Mungu mwenye mwili; kwa hili hakuna tashwishi. Kupeleleza kama kweli ni mwili wa Mungu mwenye Mwili, mwanadamu lazima aamue haya kutoka kwa tabia Yeye huonyesha na maneno Yeye hunena. Ambayo ni kusema, kama ni mwili wa Mungu mwenye mwili au la, na kama ni njia ya kweli au la, lazima iamuliwe kutokana na dutu Yake. Hivyo, katika kudadisi iwapo ni mwili wa Mungu mwenye mwili, cha msingi ni kuwa makini kuhusu dutu Yake (Kazi Yake, maneno Yake, tabia Yake, na mengine mengi), bali sio hali ya sura Yake ya nje. Mwanadamu akiona tu sura Yake ya nje, na aipuuze dutu Yake, basi hilo linaonyesha upumbavu na ujinga wa mwanadamu.”

Tazama Video:  Wimbo Mpya wa Dini | "Mungu Anapata Mwili ili tu Kumshinda Shetani na Kuwaokoa Binadamu"

 

Views: 73 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: Kupata Mwili, neno la Mungu, Njia ya uzima | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar