6:22 PM
4. Inamaanisha nini kuomba kwa kweli?

Maneno Husika ya Mungu:

Ni nini maana ya kuomba kwa kweli? Ina maana ya kuzungumza maneno yaliyo ndani ya moyo wako kwa Mungu, na kuwasiliana na Mungu baada ya kufahamu mapenzi Yake na kutegemea maneno Yake; ina maana ya kuhisi kuwa karibu na Mungu hasa, kuhisi kwamba Yeye yuko mbele yako, na kwamba una kitu cha kumwambia; na inamaanisha kuwa mwangavu hasa ndani ya moyo wako, na kuhisi kwamba Mungu ni wa kupendeza hasa. Utajisikia kutiwa moyo sana, na baada ya kusikia maneno yako ndugu zako watajisikia kufurahishwa, watahisi kwamba maneno unayosema ni maneno yaliyo ndani ya mioyo yao, maneno ambayo wangependa kusema, na kwamba kile unachosema kinawakilisha kile wanachotaka kusema. Hii ndiyo maana ya kuomba kwa kweli. Baada ya kuomba kwa kweli, moyoni mwako utahisi kuwa na amani, na kufurahishwa; nguvu ya kumpenda Mungu itaongezeka, na utahisi kwamba hakuna kitu chochote katika maisha yako yote kinachostahili au ni muhimu zaidi kuliko kumpenda Mungu—na yote haya yatathibitisha kuwa maombi yako yamekuwa yenye ufanisi.

kutoka katika “Kuhusu Desturi ya Sala” katika Neno Laonekana katika Mwili

Kiwango cha chini zaidi ambacho Mungu anahitaji kwa watu ni kwamba waweze kufungua mioyo yao Kwake. Ikiwa mwanadamu atautoa moyo wake wa kweli kwa Mungu na kusema kile kilicho ndani ya moyo wake kwa Mungu, basi Mungu yuko tayari kufanya kazi ndani ya mwanadamu; Mungu hataki moyo wa mwanadamu uliopotoka, lakini moyo wake ulio safi na mwaminifu. Ikiwa mwanadamu hasemi yaliyo moyoni mwake kwa Mungu kwa kweli, basi Mungu haugusi moyo wa mwanadamu, au kufanya kazi ndani yake. Hivyo, jambo muhimu sana kuhusu kuomba ni kusema maneno ya moyo wako wa kweli kwa Mungu, kumwambia Mungu kuhusu dosari zako au tabia ya kuasi na kujifungua kabisa kwa Mungu. Wakati huo tu ndipo Mungu atakuwa na hamu ya sala zako; la sivyo, basi Mungu atauficha uso Wake kutoka kwako.

kutoka katika “Kuhusu Desturi ya Sala” katika Neno Laonekana katika Mwili

Wakati mwingine, kumtegemea Mungu hakumaanishi kumwomba Mungu afanye kitu kwa kutumia maneno maalum, au kumwomba uongozi au ulinzi maalum. Badala yake, ni kwamba watu wanapokabiliwa na suala fulani, wanaweza kumwomba Mungu kwa kweli. Hivyo, Mungu anafanya nini pale watu wanapomwita? Wakati ambapo moyo wa mtu unatikisika na ana wazo hili: “Ee Mungu, siwezi kufanya hili mimi mwenyewe, sijui jinsi ya kufanya hivyo, na ninahisi mwenye udhaifu na uhasi,” je, Mungu anajua kuhusu hilo? Mawazo haya yanapotokea ndani ya watu, je, mioyo yao ni ya kweli? Wanapomsihi Mungu kwa kweli kwa njia hii, Mungu anakubali kuwasaidia? Licha ya ukweli kwamba huenda hawakusema neno, wanaonyesha uaminifu, na hivyo Mungu anakubali kuwasaidia. Mtu anapokabiliwa na tatizo ambalo ni gumu hasa, wakati ambapo hana mtu anayeweza kumwomba msaada na anahisi asiyejiweza, yeye huweka matumaini yake ya pekee kwa Mungu. Maombi yake yako vipi? Hali yake ya akili iko vipi? Je, ni mwaminifu? Je, kuna ughushi wakati huo? Ni wakati tu ambapo unamwamini Mungu kana kwamba ni matawi ya mwisho unayokamata ili kuokoa maisha yako, ukitumai kwamba Atakusaidia, kwamba moyo wako ni wa kweli. Ingawa huenda hujasema mengi, moyo wako tayari umesisimuka. Yaani, unatoa moyo wako wa kweli kwa Mungu, na Mungu anasikiliza. Mungu atakapoona matatizo yako, Atakupa nuru, Atakuongoza, na kukusaidia.

kutoka katika “Waumini Wanahitaji Kwanza Kubaini Mielekeo Mibaya ya

Dunia” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Sala sio jambo la kupitia urasmi wa kisheria, au kufuata utaratibu, au kukariri maneno ya Mungu, ambalo ni kusema, sala haimaanishi kuiga maneno kama kasuku na kuwaiga wengine. Katika sala, lazima umpe Mungu moyo wako, ukishiriki maneno yaliyo ndani ya moyo wako na Mungu ili uweze kuguswa na Mungu. Ikiwa maombi yako yatakuwa na matokeo, basi lazima yategemee usomaji wako wa maneno ya Mungu. Ni kwa kuomba tu katikati ya maneno ya Mungu ndipo utaweza kupokea nuru na mwangaza zaidi. Sala ya kweli huonyeshwa kwa kuwa na moyo ambao unatamani sana matakwa yaliyowekwa na Mungu, na kuwa tayari kutimiza matakwa haya; utaweza kuchukia yote ambayo Mungu huchukia, kwa msingi huo utakuwa na maarifa, na utajua na kuelewa wazi kuhusu ukweli ulioelezwa na Mungu. Kuwa na azimio, na imani, na maarifa, na njia ya kufanya mazoezi baada ya kuomba—huku tu ndiko kuomba kwa kweli, na sala kama hii tu ndiyo inaweza kuwa na ufanisi. Lakini sala lazima ijengwe juu ya msingi wa kufurahia maneno ya Mungu na kuwasiliana kwa karibu na Mungu katika maneno Yake, moyo wako ukiweza kumtafuta Mungu na kuwa na amani mbele ya Mungu. Sala kama hiyo tayari imefikia kiwango cha kuwasiliana kwa kweli na Mungu.

kutoka katika “Kuhusu Desturi ya Sala” katika Neno Laonekana katika Mwili

Natumaini kwamba ndugu wanaweza kuomba kila siku. Huku si kuzingatia mafundisho ya dini, hata hivyo, bali matokeo ambayo yanapaswa kutimizwa. Je, uko tayari kuacha usingizi kidogo na anasa, kusema sala za asubuhi wakati wa alfajiri na kisha kufurahia maneno ya Mungu? Ikiwa utaomba na kula na kunywa maneno ya Mungu, katika njia hii, kwa moyo safi, basi utakubalika zaidi na Mungu. Ikiwa unafanya hivyo kila siku, ukijizoeza kumpa Mungu moyo wako kila siku na kuwasiliana kwa karibu na Mungu, basi ufahamu wako wa Mungu utaongezeka bila shaka, na utaweza kufahamu vizuri zaidi mapenzi ya Mungu. Unapaswa kusema: “Ee Mungu! Ningependa kutimiza wajibu wangu. Ili Uweze kutukuzwa ndani yetu, na Uweze kufurahia ushuhuda ulio ndani yetu, kikundi hiki cha watu, naweza tu kutoa nafsi yangu yote kwako. Nakuomba Ufanye kazi ndani yetu, ili niweze kukupenda na kukuridhisha kwa kweli, na kukufanya Uwe lengo ambalo ninafuatilia.” Wakati ambapo unakuwa na mzigo huu, Mungu atakufanya uwe mkamilifu bila shaka; hupaswi tu kuomba kwa ajili yako mwenyewe, bali pia kwa ajili ya kutekeleza mapenzi ya Mungu, na kwa ajili ya kumpenda Yeye. Hiyo ndiyo aina ya sala ya kweli kabisa.

kutoka katika “Kuhusu Desturi ya Sala” katika Neno Laonekana katika Mwili

Kadri unavyoishi maisha ya kiroho, ndivyo moyo wako utakavyomilikiwa zaidi na maneno ya Mungu, ukishughulika na mambo haya daima na kuubeba mzigo huu daima. Baada ya hiyo, unaweza kufichua ukweli wako wa ndani kabisa kwa Mungu kupitia maisha yako ya kiroho, mwambie unachotaka kufanya, kile ambacho umekuwa ukifikiri, ufahamu wako na njia yako mwenyewe ya kuona neno la Mungu. Usizuie chochote, hata kidogo! Jizoeze kuzungumza maneno yaliyo ndani ya moyo wako kwa Mungu, mwambie ukweli, na usisite kuzungumza yaliyo moyoni mwako. Kadri unavyofanya hivi, ndivyo utakavyohisi zaidi upendo wa Mungu, na moyo wako utavutiwa zaidi na zaidi kumwelekea Mungu. Wakati ambapo hili litafanyika, utahisi kwamba Mungu ni mpenzi zaidi kwako kuliko mtu mwingine yeyote. Hutawahi kumwacha Mungu kamwe, lolote liwalo. Ikiwa utafanya aina hii ya ibada ya kiroho kila siku na usiiondoe akilini mwako, bali uichukulie kama wito wako katika maisha, basi neno la Mungu litaumiliki moyo wako. Hii ndiyo maana ya kuguswa na Roho Mtakatifu. Itakuwa kana kwamba moyo wako daima umetawaliwa na Mungu, kana kwamba kumekuwa na upendo ndani ya moyo wako daima. Hakuna anayeweza kuliondoa hilo kutoka kwako. Wakati hili litatokea, Mungu ataishi ndani yako kweli na kuwa na nafasi ndani ya moyo wako.

kutoka katika “Maisha Ya Kawaida ya Kiroho Huwaongoza Watu Kwenye Njia

Sahihi” katika Neno Laonekana katika Mwili

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Kuna matokeo mengi ambayo ushirika wa kweli na Mungu lazima utoe: Kwanza, wakati wa kuwasiliana kwa karibu na Mungu, tunaweza kuja kujua ukweli wa upotovu wetu na kiini cha asili yetu, kutimiza matokeo ya kujijua. Mbele ya Mungu, tunapaswa mara nyingi kuwazia mambo ambayo tumeyafanya ili kuona iwapo kwa kweli yanakubaliana na mapenzi ya Mungu au la, kuona tumetegemea nini kuishi. Iwapo tumeishi kwa neno la Mungu, basi huo ni ushuhuda wa kuingia katika maisha. Iwapo tumeishi kwa falsafa ya Shetani, hayo ni maonyesho ya asili potovu ya Shetani, ambayo inachukuliwa kuwa dhambi. Pili, wakati wa kuwasiliana kwa karibu na Mungu, hatutimizi tu maarifa ya kweli ya sisi wenyewe lakini tunatimiza pia maarifa ya kweli ya Mungu, ambayo ni matokeo ya kuwasiliana kwa karibu na Mungu. Baada ya kutimiza maarifa ya kweli ya Mungu, tutaanza kumcha Mungu katika mioyo yetu, kumtii Mungu katika mioyo yetu, na kumpenda Mungu katika mioyo yetu, ambayo hatimaye yataleta ndani yetu uamuzi wa kumtumikia Mungu. Haya ndiyo matokeo yanayotimizwa na kumjua Mungu, na pia ni matokeo yanayotimizwa na kuwasiliana kwa karibu na Mungu. Tusipotimiza matokeo haya katika mawasiliano yetu ya karibu na Mungu, hiyo inatosha kuthibitisha kwamba hatujaingia katika njia sahihi katika maombi yetu, na kwamba kwa kweli hatujawasiliana kwa karibu na Mungu. Watu wengine husema: “Haya, nimeomba kwa miaka mingi, kwa hivyo hiyo inamaanisha kwamba ninawasiliana kwa karibu na Mungu?” Kisha unapaswa kupima hili kulingana na matokeo haya, Je, una matokeo ya kujijua katika maombi yako kwa Mungu? Je, una matokeo ya kutafuta mapenzi ya Mungu na ukweli? Je, una matokeo ya kumtii Mungu? Je, una matokeo ya kumcha Mungu? Je, una matokeo ya kumpenda Mungu? Iwapo huna mojawapo ya matokeo haya, basi maombi yako ni matupu, hayana maana, na huwasiliani kwa kweli na Mungu kabisa.

kutoka katika “Lengo na Umuhimu wa Sala na Ushirika na Mungu” katika

Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha V

Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu

Views: 80 | Added by: flickrpinquorettfb | Tags: Sala ya kweli, upendo wa Mungu | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar