1:07 AM
Filamu za Kikristo "Wokovu" | Does Forgiveness of Sins Mean Full Salvation?

Filamu za Kikristo "Wokovu" | Does Forgiveness of Sins Mean Full Salvation?

Wokovu ni nini? Wale wanaoamini katika Bwana Yesu hufikiria kwamba ikiwa wataomba kwa dhati kwa Bwana, waungame dhambi zao, na kutubu, dhambi zao zitasamehewa, na watapewa wokovu, na Bwana Atakapokuja, wao watainuliwa moja kwa moja hadi katika ufalme wa mbinguni. Lakini je, wokovu kweli ni rahisi hivyo?

Shujaa katika filamu, Xu Zhiqian, ameamini katika Mungu kwa miaka mingi, akijitolea kwa shauku kwa Mungu, na kuacha kila kitu ili kutenda wajibu wake. Kwa ajili ya hili, alikamatwa na kuteswa na Chama cha Kikomunisti cha China. Baada ya kuachiliwa kutoka gerezani, aliendelea kutekeleza wajibu wake, alipata uzoefu kidogo wa vitendo, na mahubiri yake na kazi ilitatua matatizo ya matendo kwa ndugu zake. Baadaye, mkewe pia alikamatwa, lakini hakulalamika, kuwa hasi, au kusambaratika.... Yote haya yalimshindia pongezi na sifa kutoka kwa ndugu zake. Xu Zhiqian anaamini kwamba ana uhalisi wa ukweli na kwamba hakuna tatizo kuingia katika ufalme wa mbinguni. Lakini punde tu, jaribio lisilotarajiwa lilimjia—mkewe anakufa chini ya mateso ya polisi wa CCP. Xu Zhiqian, akiwa na wasiwasi, ana dhana, kutoelewana, na malalamishi kuhusu Mungu, vilevile mawazo ya maasi dhidi ya na usaliti kwa Mungu.... Baadaye, wakati anapogundua anamsaliti Mungu, anaanza kutafakari, na kustaajabu kama watu ambao, kama yeye, hupitia majaribio na kisha kulalamika, hukosa kumwelewa Mugu, na humsaliti Mungu hakika huokolewa. Je, wao kweli wanastahili kuingia katika ufalme wa Mungu?

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Views: 135 | Added by: hatat1946 | Tags: Yesu, Wokovu, Mungu | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar