9:36 PM
Kutembea Katika Njia Ng’avu ya Maisha

Wokovu wa Mungu: Kutembea Katika Njia Ng’avu ya Maisha

Xie Li, Marekani

Zamani nilikuwa mtu ambaye angefuata mitindo ya dunia, nilitaka kujiachilia kwa maisha ya anasa, na nilijali tu kuhusu anasa za mwili. Mara nyingi ningeenda na rafiki zangu kwa KTV usiku mzima, ningeenda matembezi kwa motokaa katikati ya usiku, ningeenda kuvua samaki katika bahari, na kusafiri pande zote nikitafuta vyakula vizuri. Ningeona wengine walionizunguka, na wao wote pia walikuwa wanajizatiti kula vizuri, kuvaa vitu vizuri, na kufurahia vitu vizuri. Nilihisi kwamba hivi vilikuwa vitu ambavyo mwanadamu lazima afanye kazi kuvitimiza katika maisha yake, kwamba hii ndiyo maana lazima ufanye kazi kwa bidii kupata pesa, kwamba hili ndilo lengo katika maisha ambalo kila mtu anapaswa kuwa nalo. Ni kwa kuwa na vitu hivi pekee ndipo maisha hayangekuwa bure. Ili kupata vitu hivi, sikujali ilinibidi nisafiri umbali gani, hivyo nilivuka bahari kuja Marekani, na baada ya kupambana kwa miaka kadhaa, nilifungua biashara yangu mwenyewe. Nilikuwa na gari langu mwenyewe na nyumba yangu mwenyewe. Nilikuwa nikiishi maisha yaliyobarikiwa ambayo nilikuwa nimeota kuyahusu. Kila siku ningekula, kunywa na kufuatilia anasa hadi nilipokuwa nimetosheka na moyo wangu ulikuwa umeridhika. Nilidhani kwamba ilikuwa tu kwa kuishi kwa njia hii ndiyo maisha yalikuwa na maana yoyote, na hiyo ni mpaka nilipopokea kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Ni baada tu ya kupitia hukumu na kuadibu kwa Mungu ndipo nilipata utambuzi wa maisha muhimu kwa kweli ni yapi, na kisha nilianza kutembea katika njia ng’avu ya maisha.

Kutembea Katika Njia Ng’avu ya Maisha | Kanisa la Mwenyezi Mungu

 

Mnamo Mei 2016, mke wangu alinipa injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu. Kwa kusoma neno la Mwenyezi Mungu, nilipata utambuzi wa mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka elfu sita wa kuwaokoa wanadamu, na pia nilipata kuelewa kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Yehova Mungu ambaye aliwaongoza Waisraeli kutoka Misri, kwamba Yeye pia ni Bwana Yesu ambaye alikomboa wanadamu kwa kutundikwa msalabani, na kwamba sasa Amerudi katika mwili kuonyesha ukweli na kutekeleza kazi ya kuhukumu, kutakasa na kumwokoa mwanadamu…. Kabla ya muda mrefu sana, nilianza kushiriki katika maisha ya kanisa katika Kanisa la Mwenyezi Mungu na hapo nilipata kuwasiliana na ndugu wa Kanisa la Mwenyezi Mungu, niliona kwamba wote walikuwa waaminifu sana, hakukuwa na kujifanya ama maoni matupu katika maneno waliyozungumza, na kuwa katika mawasiliano na wao kulinipa hisia ya ukombozi ambayo sikuwa nimewahi kuhisi awali.

Nilipoanza kuhudhuria mikutano ya kanisa nilijihisi mchangamfu, na nilitaka kukusanyika pamoja na ndugu na kufuatilia vizuri ukweli na kufuatilia mabadiliko katika tabia ya maisha yangu. Lakini, kwa sababu hadi wakati huo nilikuwa nimetamani raha za mwili na kufuatilia anasa za maisha, singeweza kujisaidia hata ingawa nilikuwa na tamaa ya kukusanyika na kufuatilia ukweli. Wakati mmoja rafiki aliponialika kwenda kula mlo mkuu wa usiku, ilikuwa wakati sawa na mkutano wa kanisa, jambo ambalo lilinifanya kuhisi mgongano mkubwa ndani. Niende ama nisiende? Nilijiwazia swali hili: Imekuwa muda mrefu tangu nilipoenda kufurahia. Si rahisi kwa rafiki yangu kunialika leo, kwa hivyo napaswa kuenda. Hata hivyo, rafiki zangu hawanialiki kwenda nje kila siku, na ninaweza kwenda kwa mkutano wa kanisa wakati ujao tu. Hivyo, nilidai kwamba nilikuwa na kitu cha kufanya na kuachana na mpango wangu wa kwenda kwa mkutano wa kanisa na badala yake nilienda kula mlo mkuu wa usiku. Tulikula, tukanywa pombe, tukaenda KTV, lakini nilipokuwa nikirudi nyumbani sikuhisi furaha yoyote ndani yangu. Katika kina cha moyo wangu nilihisi aina fulani ya utupu usioweza kuelezeka, na pia nilikuwa na hisia za hatia. Nilikumbuka siku za nyuma. Nilipokuwa nikila na rafiki zangu na wanakijiji wenza wote walikuwa wachangamfu kabisa kwangu mezani, lakini pasi na mimi kujua walikuwa wakitafakari, wakipanga njama, wakijaribu kufikiri jinsi ya kuchukua pesa zangu kwa ulaghai. Kuwashughulikia wote kulinifanya mchovu sana. Singeweza kabisa kupata yeyote wa kuzungumza naye kuhusu mambo niliyojali kuhusu. Nilienda nje leo na kunywa na kula hadi nilipotosheka kabisa, na pia nimeridhisha rafiki zangu, lakini kweli nilipata nini? Nilihisi mtupu na asiyejiweza, nilihisi kwamba nilikuwa nimemsikitisha Mungu, na nilihisi majuto kwa ndugu zangu.

Hata hivyo, utupu huu katika roho yangu, hisia hii ya kujilaumu bado haingeweza kuniweka huru kutoka kwa ushawishi wa dunia ya anasa za ashiki. Katika moyo wangu bado nilikuwa natamani kujiachilia kwa maisha ya anasa, kwa vitu ambavyo ni vya mwili, lakini Mungu alipanga vitu na kuweka hali katika njia ya vitendo kubadili maoni haya yenye makosa kuhusu kufuatilia. Siku ya Taifa ikiwa inakaribia, mke wangu alinipendekezea: “Tuwe tu na sherehe rahisi, kisha na muda wowote ambao tutakuwa tumesalia nao tunaweza kusoma neno la Mungu zaidi na kutazama video fulani kutoka kwa familia ya Mungu ili tuweze kutayarishwa na ukweli zaidi na kuelewa neema ya Mungu ya wokovu.” Lakini kwa kweli sikuyazingatia maneno ya mke wangu, na badala yake nikaanza kufanya matayarisho ya jinsi ningesherehekea sikukuu. Nilichagua kwa makini njia gani ningechukua, na nikaenda sokoni na kununua vyakula vyote na vitu vingine ambavyo ningehitaji. Niliamua kuenda na mke wangu ufukoni mwa bahari na kuchoma nyama yetu kiasi. Kwa hivyo wakati Siku ya Taifa ilipofika nilimchukua mke wangu nami na tukaelekea kwa furaha tukiwa garini. Hata hivyo, kila kitu hakikuwa kinaenda kulingana na mpango, kulikuwa na msongamano wa magari barabarani njia nzima, na katikati ya safari hiyo tuligundua kwamba mfumo wa gari wa kutusaidia kujua tulipokuwa (GPS) haukuwa ukifanya kazi vizuri hivyo tulikuwa tukienda njia mbaya. Haikuwa rahisi kufika mwisho wa safari yetu, na mwishowe, mara tulipofika ufukoni mwa bahari upepo ulikuwa mkali sana, ukitufanya tusiweze kuchoma nyama yetu. Hivyo mke wangu aliniomba kugeuza gari na kurudi nyumbani, lakini sikuwa tayari kufanya hivyo. Nilisisitiza kwamba tuendelee kuendesha gari tukitafuta bustani ya karibu ambapo tungeweza kuchoma nyama yetu, lakini bustani tatu tulizoenda zilikuwa zimejaa watu, na hata hakukuwa na popote pa kuegesha gari. Ni baada ya hapa tu ndipo niligeuka bila kutaka na kuendesha gari kurudi nyumbani. Njia ya kuelekea nyumbani ilikuwa na msongamano mkubwa wa magari kama awali. Awali tulikuwa tumetoka ili kwenda kuchoma nyama kwa ajili ya chakula cha mchana, lakini sasa tayari ilikuwa baada ya saa kumi jioni na bado hatukuwa tumepika chochote. Tulikuwa tukihisi njaa sana. Kwa kawaida nahisi kwamba niko sahihi na najiamini sana, na wakati huo sikuwa na hamaki, na hakukuwa na chochote nilichotaka kusema. Nilikaa tu kimya na kuendesha gari kurudi nyumbani nikihisi huzuni. Ilikuwa wakati huu ndipo gari lililokuwa mbele yangu kwa ghafla lilifunga breki ghafla, na kwa hiyo ilinibidi kwa haraka nifunge yangu. Ingawa sikuligonga hilo gari lililokuwa mbele yangu, niligongwa na gari lililokuwa nyuma yangu. Kwa bahati nzuri, hakuna aliyeumia, na ni upande wa juu wa gari tu ulioumia kidogo. Nilijua kwamba Mungu alikubali tukio hili kutendeka, sikutaka kumlaumu huyo dereva mwingine, na hivyo niliendesha gari kutoka hapo tu. Nilijiwazia: Ala, hiyo mipango yote ya makini niliyopanga kwa ajili ya sikukuu ilikuwa jitihada bure, hakika ni kweli kwamba mipango haiwezi kwenda sawia na mabadiliko, na kila kitu kinapangwa na Mungu. Kwa kweli singetoka nje leo kujiachilia kwa anasa za maisha. Singetegemea tabia yangu mwenyewe!

Tulipofika nyumbani mke wangu nami tulisoma pamoja vifungu kadhaa kutoka kwa neno la Mungu: “Watu zaidi wanachukulia rekodi za kazi ya Mungu na maneno Yake wakati wa enzi ya Agano la Kale kuwa hadithi na hekaya. Kwa mioyo yao, watu wanakuwa wasiojali heshima na ukubwa wa Mungu, kwa imani kwamba Mungu yupo na anatawala kila kitu. Kusalia kwa mwanadamu na majaliwa ya nchi na mataifa si muhimu kwao tena. Mwanadamu anaishi katika dunia tupu akijishughulisha tu na kula, kunywa, na ufuatiliaji wa furaha. … Watu wachache wanashughulika kutafuta Afanyapo Mungu kazi Yake leo, ama kutafuta jinsi Anavyoongoza na kupanga majaliwa ya mwanadamu” (“Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Ambao unaendelea kuwa hivyo zaidi na zaidi. Watu wanapotazama ulimwengu, mioyo yao inavutiwa nao, na wengine hawawezi kujinasua kutoka kwa ulimwengu…. Usipojitahidi ili kuendelea mbele, na huna maadili, utapeperushwa na wimbi hili lenye dhambi” (“Utendaji (2)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mwenyezi Mungu yanafanya kiini cha mitindo ya dunia kuwa dhahiri na wazi sana. Mitindo ya dunia ni Shetani tu kumshawishi mwanadamu na kumfanya mpotovu. Ni hila na njama tu zinazonuiwa kumteketeza mwanadamu. Shetani hutumia tu kula, kunywa, kufuatilia kwa anasa na vitu vingine vinavyopatana na mwili ili kumdanganya mwanadamu na kumnyima mwanadamu uhuru. Punde moyo wa mwanadamu unapomilikiwa na vitu hivi ambavyo ni vya mwili hataelekea tena kufuatilia mambo mema, na atakuwa mbali zaidi na zaidi na Mungu, ambalo litamsababisha kuteketezwa na kutekwa na Shetani. Kupitia kusoma neno la Mungu nilipata kutambua kwamba maoni yangu kuhusu kufuatilia yote yalikuwa si sahihi kabisa. Bila kujali ninachojihusisha nacho, iwe kula, kunywa, kufuatilia anasa za mwili au kutafuta maisha ambapo nipo juu ya wengine, vitu hivi vyote ni matokeo ya Shetani kupotosha jamii ya binadamu. Nimethibitisha kupitia kwa uzoefu wangu mwenyewe kwamba mtu anapofuatilia vitu hivi ambavyo ni vya Shetani atakuwa tu mpotovu zaidi na zaidi, na mbaya na zaini zaidi na zaidi. Itaongeza tu kwa tamaa, ubinafsi, uovu na udanganyifu wake. Atakuwa akiishi katika dhambi, na hatakuwa na ubinadamu wa kawaida. Hata mwanadamu akifurahia vitu hivi zaidi na zaidi, hata mwanadamu apate vitu hivi zaidi na zaidi, mwishowe, bado atakuwa katika nafasi tupu. Kama mwanadamu angemiliki vitu hivi vyote lakini hakuja mbele ya Mungu, bado maisha yangekuwa bure, na yangekuwa bila maana ama thamani. Ni kwa kuja mbele ya Mungu pekee na kumwamini Mungu na kumwabudu Mungu ndipo mwanadamu atakuwa akitembea katika njia ya kuisha maisha ya kufaa, na hapo tu ndipo mwanadamu atajiweka huru kutoka kwa maisha ya utupu na uovu. Hivyo, niliamua kubadili jinsi naishi maisha yangu na kutembea katika njia sahihi ya maisha.

Nilipoona ndugu zangu wakijitumia kwa vitendo kwa ajili ya Mungu, nilipoona kujitolea kwao kutekeleza wajibu wao na kufuatilia kwao maisha yenye maana mimi pia basi nilihisi hamu ya kufuatilia vitu hivi na kuishi jinsi watu halisi huishi kama inavyohitajika na Mungu. Kwa hivyo, kwa kuongezea mikutano ya kawaida, pia nilitaka kupata wakati wa kutekeleza wajibu wangu binafsi. Ilikuwa wakati huu ambapo kanisa lilinipangia wajibu fulani. Walitaka niendeshe gari kupeleka ndugu zetu wawili wa kike mahali fulani, na walitaka niwachukue tena wiki iliyofuata. Mara ya kwanza wajibu huu ulipokabidhiwa kwangu, niliukubali kwa furaha. Lakini wakati ndugu walionipa kazi hii walipoondoka, nilianza kusitasita na hata kuhisi majuto fulani: “Aa, siku ninayopaswa kupeleka ndugu hawa wa kike inapaswa kuwa siku yangu ya kupumzika kazi, na wiki ijayo lazima niende kuwachukua. Itanilazimu kuamka mapema sana siku hizi mbili. Haijalishi safari ni ndefu vipi, lakini la muhimu ni kwamba kwa kweli ni rahisi kwa njia hiyo kusongamana na magari. Ni heri kwenda mapema asubuhi kwa sababu wakati huo kuna magari machache, lakini nani ajuaye nitakwama katika msongamano wa magari kwa muda upi nikirudi? Wakati wangu wote utapotezwa nikiwa katika huo msongamano, na sitakuwa na siku yangu ya kupumzika kazi….” Bibi yangu aliposikia nikilalamika hivi, alishiriki na mimi: “Kutekeleza wajibu wako si rahisi kama ulivyodhania. Kwa hakika kutahusisha wewe kutia ukweli katika vitendo. Kutenda ukweli ni kuunyima mwili, na kunamaanisha utapitia taabu na kulipa gharama. Fikiria, hapo nyuma ulikuwa ukienda nje na kunywa, kula na kufuatilia anasa, na hata kama kwa kweli hukufurahia baada ya siku ya kuchosha, kamwe hungelalamika. Lakini sasa umepewa kazi na unahitaji kutumia muda wako fulani kwa kazi hiyo, na unahitaji kutembea njia iliyo na taabu, lakini katika moyo wako hutaki kufanya hili. Wajibu huu, ingawa kwa nje unaonekana kuwa kitu ambacho ulipangiwa na ndugu zako, kwa kweli hutekelezi wajibu huu kwa sababu ya mtu fulani, lakini ni kwa ajili ya kumridhisha Mungu na kulipiza upendo wa Mungu. Wajibu huu umepewa leo, huyu ni Mungu akikuinua, na huu ni upendo wa Mungu ukija chini kwako. Unapaswa kuhifadhi hili kwa upendo mkubwa. Usijiwachie majuto katika wajibu wako wa kwanza.” Baada ya yeye kusema hili, alinisomea kifungu cha neno la Mungu: “Unafaa kulipa gharama kwa kila unachokifanya. Bila mateso ya kweli, huwezi kumridhisha Mungu, hata haikaribii kumridhisha Mungu, hakutakuwa na kitu ila maneno matupu! Je, haya maneno matupu yaweza kumridhisha Mungu? Wakati Mungu na Shetani wanapigana katika milki ya kiroho, utamridhishaje Mungu, na utasimamaje imara katika ushuhuda wako Kwake? Unapaswa kujua kuwa kila kitu unachokipitia ni majaribu makubwa na ndipo Mungu hukuhitaji kuwa na ushuhuda. Kwa nje yataonekana kama mambo madogo; lakini haya mambo yakitendeka huonyesha kama unampenda Mungu au la. Ikiwa unampenda, utaweza kusimama imara katika ushuhuda wako Kwake, na ikiwa hujaweka upendo Wake katika vitendo, hili linaonyesha kuwa wewe si Mtu ambaye anapenda kuuweka ukweli katika vitendo, kwamba huna ukweli, huna uzima, kuwa wewe ni makapi! Mambo huwatokea watu wakati Mungu anawataka wasimame imara katika ushuhuda wao Kwake. Hakuna kubwa lililokutendekea kwa sasa, na huna ushuhuda mkubwa, lakini kila chembe ya maisha yako ya kila siku inahusiana na ushuhuda kwa Mungu” (“Kumpenda Mungu Tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili).

Nilipomaliza kusoma neno la Mwenyezi Mungu, nilipomaliza kusikiza maneno ya mke wangu, hapo nilitambua kwamba Mungu kunipa wajibu huu ulikuwa Yeye kunipa jaribio halisi, kuona iwapo ningeweza kumridhisha Mungu na kuvumilia taabu au la. Lakini nilichofichua kilikuwa kwamba nilifikiri tu maslahi ya mwili wangu mwenyewe, kwamba nilifikiri faida na hasara zangu binafsi pekee, kwamba sikuwa tayari kuteseka na kulipa gharama, kwamba badala yake nilikuwa nikilalamika kuhusu vitu. Niliona kwamba nilikuwa mbinafsi kabisa, kwamba katika moyo wangu tamaa za mwili kama kunywa, kula na anasa zingine tayari zilikuwa zimepita hadhi ya Mungu katika moyo wangu. Nilikuwa na furaha mno kutumia chochote nilichokuwa nacho, kulipa gharama yoyote ili kula, kunywa na kufuatilia anasa, lakini nilipopewa wajibu uliohitaji mimi kutumia wakati wangu kwa ajili ya Mungu nilianza kukokotoa faida na hasara zangu mwenyewe, na sikuwa tayari kutenda ukweli ili kumridhisha Mungu. Fikira na vitendo hivi vyangu vingemfanya Shetani anicheke, na kutoniruhusu kuwa shahidi mbele za Mungu. Baada ya mimi kuja kuelewa vitu hivi nilikuja haraka mbele ya Mungu na kuomba kwamba Aweze kunipa hiari kuhakikisha kwamba ningeweza kuunyima mwili wangu na kutomfuata Shetani tena, ili ningeweza kuwa shahidi mbele za Mungu na kumshinda Shetani katika mapambano ya kiroho niliyokuwa ndani! Baada ya mimi kubadili mtazamo wangu kuhusu wajibu huo, katika ushirikiano wangu wa vitendo, kwa kweli niliona baraka ya Mungu. Haikujalisha iwapo ilikuwa wakati nilipokuwa nikipeleka ndugu wa kike nyumbani kwao ama kuwachukua tena, sikupatana na misongamano mikubwa ya magari pande zote mbili. Lilikuwa limezidi fikira zangu kabisa, na dhana zangu kwa kweli zilipingwa. Nilipitia kwa mara ya kwanza hisia ya amani na furaha ambayo ililetwa na kutekeleza wajibu huo, na pia niliona kwamba wakati watu huunyima mwili na kutenda kumridhisha Mungu, Mungu hatawaandalia tu njia, lakini pia Atawaruhusu kuelewa ukweli na kuona vitendo Vyake. Ghafla nilihisi kwamba hili lilinifanya kuwa na furaha zaidi kuliko kwenda likizoni ama kula chakula badhirifu. Kama ilivyo, kufanya hivi katika siku ya kupumzika kazi kwa kweli si kupoteza wakati. Kwa kweli ni kwa maana kabisa!

Ndani ya huu uzoefu wa vitendo niliweza kujijulia ladha tamu ya kuunyima mwili na kutekeleza wajibu ili kumridhisha Mungu. Niliona kwamba yote Mungu hufanya ni ili kuniokoa kutoka kwa ushawishi mwovu wa Shetani, ili siku moja karibuni sana niweze kutembea katika njia sahihi ya kufuatilia ukweli. Vitu hivi vyote ni upendo na wokovu wa Mungu. Siku chache zilipita na kisha nikapigiwa simu na mmoja wa ndugu wa kiume. Aliniuliza iwapo nilikuwa na hiari ya kuenda katika jimbo lingine kuwachukua ndugu fulani au la, na nilikubali kufanya hilo bila kusita hata kidogo. Baada ya kukubali hili sikuhisi malalamiko. Nilikuwa tayari kabisa na mwenye furaha kufanya kile nilichohitajika kufanya, na safari yote ikaendelea bila kuzuiliwa. Baada ya kuwafikisha ndugu mwisho wa safari yao salama, nilijivunia sana, kwa sababu hii ilikuwa mara ya kwanza kwangu kutekeleza wajibu kwa hiari, bila uchafu wowote. Hili lilinifundisha pia kwamba kutekeleza wajibu ambao kiumbe anapaswa kutekeleza ni kitu cha maana sana mtu anaweza kufanya kwa kweli. Sikuwa nataka tena kunywa, kula na kufuatilia anasa, sikuwa nataka tena kufuatilia anasa za mwili, na yote niliyotaka kufanya ilikuwa kufuatilia ukweli, kukubali ukweli na kutenda ukweli, ili siku moja karibuni niweze kuwa mtu ambaye kwa kweli anampenda Mungu. Mambo haya madogo katika maisha yangu yamepata kunibadili kwa njia ambazo sitambui. Maisha yangu hayako mabovu na potovu tena kama yalivyokuwa siku za nyuma. Nimeanza kubadilika na kufanya kazi kwa vitendo kufanikisha mambo. Ni kana kwamba nimeanza sura mpya kabisa katika maisha yangu. Katika moyo wangu nahisi utamu na furaha ambayo sijawahi kupitia awali, na ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniongoza katika njia ng’avu ya maisha. Utukufu wote uwe kwa Mwenyezi Mungu!

Chanzo: Kutembea Katika Njia Ng’avu ya Maisha 

Views: 120 | Added by: hatat1946 | Tags: Wokovu-wa-Mungu | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar